Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 9:5 - Swahili Revised Union Version

5 Aiondoaye milima, nayo haina habari, Akiipindua katika hasira zake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Yeye huiondoa milima bila yenyewe kutambua, huibomolea mbali kwa hasira yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Yeye huiondoa milima bila yenyewe kutambua, huibomolea mbali kwa hasira yake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Yeye huiondoa milima bila yenyewe kutambua, huibomolea mbali kwa hasira yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.

Tazama sura Nakili




Yobu 9:5
23 Marejeleo ya Msalaba  

Kaburi li wazi mbele yake, Uharibifu nao hauna kifuniko.


Huunyoshea mwamba wa gumegume mkono wake; Huipindua milima hata misingi yake.


Kwa sababu hiyo yeye huyatafiti matendo yao; Naye huwapindua usiku, wakaangamia.


Mwaga mafuriko ya hasira zako, Ukamtazame kila mtu mwenye kiburi, ukamdhalilishe.


Ni nani aliyetangulia kunipa hata nimlipe? Kila kilicho chini ya mbingu nzima ni changu.


Enyi milima, ndio mruke kama kondoo dume? Enyi vilima, kama wana-kondoo?


Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.


Nchi ilitetemeka Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.


Ni nani aliyeyapima maji kwa konzi ya mkono wake, na kuzikadiria mbingu kwa shubiri, na kuyashika mavumbi ya dunia katika pishi, na kuipima milima kwa uzani, na vilima kama kwa mizani?


Milima hutetema mbele zake, navyo vilima huyeyuka; nayo dunia huinuliwa mbele za uso wake, naam, dunia na wote wakaao ndani yake.


Ni nani awezaye kusimama mbele za ghadhabu yake, naye ni nani awezaye kukaa katika ukali wa hasira yake? Hasira yake kali humwagwa kama moto, nayo majabali yapasuliwa na yeye.


Milima ilikuona, ikaogopa; Gharika ya maji ikapita; Vilindi vikatoa sauti yake, Vikainua juu mikono yake.


Akasimama na kuitikisa dunia; Akatazama, mataifa yakatetemeka; Na milima ya zamani ikatawanyika; Vilima vya kale vikainama; Miendo yake ilikuwa kama siku za kale.


Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie.


Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka.


Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hadi chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;


kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi; na njaa na tauni mahali pengi; na mambo ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.


Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, mimi si kitu.


Na katika saa ile palikuwa na tetemeko kuu la nchi, na sehemu ya kumi ya mji ikaanguka; wanadamu elfu saba wakauawa katika tetemeko lile. Na waliobakia wakaingiwa na hofu, wakamtukuza Mungu wa mbingu.


Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo