Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yobu 12:4 - Swahili Revised Union Version

4 Mimi ni mtu wa kuchekwa na jirani yake, Ni mtu niliyemwita Mungu, naye akanijibu; Huyo mwenye haki, aliye mtimilifu, amekuwa ni kicheko.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu: Mimi niliyemwomba Mungu na akanijibu; mimi niliye mwadilifu na bila lawama, nimekuwa kichekesho kwa watu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu: Mimi niliyemwomba Mungu na akanijibu; mimi niliye mwadilifu na bila lawama, nimekuwa kichekesho kwa watu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 Nimekuwa kichekesho kwa rafiki zangu: mimi niliyemwomba Mungu na akanijibu; mimi niliye mwadilifu na bila lawama, nimekuwa kichekesho kwa watu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 “Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!

Tazama sura Nakili




Yobu 12:4
26 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha?


Katika mawazo yake huyo aliye na raha mna kudharau balaa; Tayari kwa ajili ya wenye kuteleza miguu.


Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu, Najua ya kuwa mimi ni mwenye haki.


Wamenifumbulia vinywa vyao; Wamenipiga shavuni kwa kunitukana; Hukutana pamoja juu yangu.


Rafiki zangu hunidharau; Lakini jicho langu humwagia Mungu machozi;


Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka, Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao.


Amenifanya niwe mithali kwa watu; Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi.


Niacheni, nami pia nitanena; Tena nikiisha nena, zidini kudhihaki.


Lakini sasa hao walio wadogo wangu hunifanyia mzaha, Ambao baba zao ningewadharau hata kuwasimamia mbwa wa kundi langu.


Na sasa mimi nimekuwa wimbo wao, Naam, nimekuwa simo kwao.


Je! Ni mtu gani mfano wa Ayubu, Anywaye mzaha kama maji?


Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu; Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.


Mimi ni mkamilifu; siangalii nafsi yangu; Naudharau uhai wangu.


Bila heshima walinidhihaki kupindukia, Wakanisagia meno yao.


Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;


Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA; Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.


Ee BWANA, umenihadaa, nami nimehadaika; wewe una nguvu kuliko mimi, ukashinda; nimekuwa kitu cha kuchekesha, mchana kutwa; kila mtu hunidhihaki.


Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.


Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.


Wakasokota taji la miiba, wakaliweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kulia; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!


akawaambia, Ondokeni; kwa maana msichana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.


Wakamcheka sana. Naye alipokwisha kuwatoa nje wote, akamtwaa babaye yule kijana na mamaye, na wale walio pamoja naye, akaingia ndani alimokuwamo yule kijana.


Basi Mafarisayo, ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia hayo yote, wakamdhihaki.


Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena kuhusu habari hiyo.


wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa minyororo, na kwa kutiwa gerezani;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo