Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Yeremia 48:11 - Swahili Revised Union Version

11 Moabu amestarehe tangu ujana wake, naye ametulia juu ya sira zake, wala hakumiminwa kutoka chombo kimoja kutiwa chombo kingine, wala hakwenda kufungwa; kwa hiyo ladha yake anakaa nayo, wala harufu yake haikubadilika.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika gudulia. Hajamiminiwa toka chombo hata chombo, hajapata kuchukuliwa uhamishoni. Kwa hiyo yungali na ladha yake, harufu yake nzuri haijabadilika kamwe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika gudulia. Hajamiminiwa toka chombo hata chombo, hajapata kuchukuliwa uhamishoni. Kwa hiyo yungali na ladha yake, harufu yake nzuri haijabadilika kamwe.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika gudulia. Hajamiminiwa toka chombo hata chombo, hajapata kuchukuliwa uhamishoni. Kwa hiyo yungali na ladha yake, harufu yake nzuri haijabadilika kamwe.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 “Moabu amestarehe tangu ujana wake, kama divai iliyoachwa kwenye machujo yake, haikumiminwa kutoka chombo kimoja hadi kingine, hajaenda uhamishoni. Kwa hiyo ana ladha ile ile kama aliyokuwa nayo, nayo harufu yake haijabadilika.

Tazama sura Nakili




Yeremia 48:11
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha, Na dharau ya wenye kiburi.


Mungu atawalaye tangu milele atanisikia; Na kuwaadhibu, maana hawajirekebishi, Wala kumcha Mungu.


Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.


Tumesikia habari za kiburi cha Moabu, ya kwamba ni mwenye kiburi kingi; habari za majivuno yake, na kiburi chake, na ghadhabu yake; majivuno yake si kitu.


Dunia hii itafanywa tupu kabisa, na kuharibiwa kabisa; maana BWANA amenena neno hilo.


Na katika mlima huu BWANA wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.


Mimi nilisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako tangu ujana wako, kutoitii sauti yangu.


Basi, tazama, siku zinakuja, asema BWANA, ambazo nitatuma kwake wamiminao, nao watammimina, nao watamwaga vyote vilivyomo vyomboni mwake, na kuzivunja chupa zake vipande vipande.


Tumesikia habari za kiburi cha Moabu; Ya kuwa ana kiburi kingi; Ujeuri wake, na kiburi chake, na majivuno yake, Na jinsi alivyojitukuza moyoni mwake.


Nebukadneza, mfalme wa Babeli, amenila, ameniponda, amenifanya kuwa chombo kitupu; amenimeza kama joka, amelijaza tumbo lake vitu vyangu vya anasa; amenitupa


Amekuwa utupu, na ukiwa, na uharibifu; hata moyo unayeyuka, na magoti yanagonganagongana; moyoni kote mna uchungu, na nyuso za wote zimekuwa nyeupe kwa hofu.


Kwa maana BWANA anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao.


Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya masira yao; wasemao katika mioyo yao, BWANA hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.


Nami ninayakasirikia sana mataifa yanayostarehe; kwa maana mimi nilikuwa nimekasirika kidogo tu, nao wakayazidisha maafa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo