Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Walawi 15:2 - Swahili Revised Union Version

2 Haya, semeni na wana wa Israeli, mkawaambie, Mtu yeyote atakapokuwa na kisonono na kutokwa usaha mwilini mwake, atakuwa najisi kwa ajili ya kisonono chake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 “Waambieni Waisraeli hivi: Mwanamume yeyote akitokwa na usaha, usaha huo wamfanya kuwa najisi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 “Waambieni Waisraeli hivi: Mwanamume yeyote akitokwa na usaha, usaha huo wamfanya kuwa najisi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 “Waambieni Waisraeli hivi: Mwanamume yeyote akitokwa na usaha, usaha huo wamfanya kuwa najisi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 “Semeni na Waisraeli mwaambie: ‘Wakati mtu yeyote anapotokwa na usaha mwilini, usaha huo ni najisi.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Haya, semeni na wana wa Israeli, mkawaambie, Mtu yeyote atakapokuwa na kisonono na kutokwa usaha mwilini mwake, atakuwa najisi kwa ajili ya kisonono chake.

Tazama sura Nakili




Walawi 15:2
15 Marejeleo ya Msalaba  

na imwangukie Yoabu kichwani pake, na nyumba yote ya babaye, tena hiyo nyumba ya Yoabu isikose kuwa na mtu mwenye kutoka damu, au aliye na ukoma, au mwenye kutegemea fimbo, au mwenye kuanguka kwa upanga au mwenye kuhitaji chakula.


Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, Na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu Wawajulishe wana wao,


Kisha BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,


Na unajisi wake katika kisonono chake ni huu; kama mwili wake unachuruzika kisonono chake, au kama kisonono chake kimezuiwa mwilini mwake, ni unajisi wake.


Mtu yeyote wa kizazi cha Haruni aliye na ukoma, au kisonono; asile katika vitu vitakatifu, hata atakapokuwa safi. Tena mtu yeyote atakayekinusa kitu kilicho na unajisi kwa sababu ya wafu, au mtu ambaye shahawa humtoka;


au kama akiugusa uchafu wa binadamu, uchafu wowote ambao kwao amepata unajisi, bila kujua, hapo apatapo kulijua, ndipo atakapokuwa na hatia;


Waamrishe wana wa Israeli kwamba wamtoe kila mwenye ukoma kambini, na kila mtu aliye na kisonono, na kila aliye najisi kwa ajili ya maiti;


Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.


Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,


Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu yeyote,


Kwafaa sana kwa kila njia. Kwanza kwa kuwa wamekabidhiwa mausia ya Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo