Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Nahumu 3:18 - Swahili Revised Union Version

18 Wachungaji wako wanalala usingizi, Ee mfalme wa Ashuru; watu wako wenye heshima wamepumzika; watu wako wametawanyika juu ya milima, wala hapana mtu wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Ewe mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala, waheshimiwa wako wamesinzia. Watu wako wametawanyika milimani, wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Ewe mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala, waheshimiwa wako wamesinzia. Watu wako wametawanyika milimani, wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Ewe mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala, waheshimiwa wako wamesinzia. Watu wako wametawanyika milimani, wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia; wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia; wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika. Watu wako wametawanyika juu ya milima bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

18 Wachungaji wako wanalala usingizi, Ee mfalme wa Ashuru; watu wako wenye heshima wamepumzika; watu wako wametawanyika juu ya milima, wala hapana mtu wa kuwakusanya.

Tazama sura Nakili




Nahumu 3:18
13 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Niliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji. BWANA akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.


Hofu na woga zimewaangukia; Kwa uweza wa mkono wako wanakaa kimya kama jiwe; Hata watakapovuka watu wako, Ee BWANA, Hata watakapovuka watu wako uliowanunua.


Basi, itakuwa kama vile paa aliyetishwa, na kama kondoo wasio na mtu wa kuwakusanya; kila mtu atageukia watu wake; nao watakimbia, kila mtu aende nchi yake mwenyewe.


Haya, shuka, keti mavumbini, Ewe bikira, binti Babeli; Keti chini pasipo kiti cha enzi, Ewe binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.


Basi, BWANA wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, mimi nitamwadhibu mfalme wa Babeli, na nchi yake, kama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru.


Wakiingiwa na ukali, nitawafanyia karamu yao, nami nitawalevya, wapate kufurahi, na kulala usingizi wa milele, wasiamke tena, asema BWANA.


Nami nitawalevya wakuu wake, na watu wake wenye hekima, watawala wake, na makamanda wake, na mashujaa wake; nao watalala usingizi wa milele, wasiamke, asema Mfalme, BWANA wa majeshi, ambaye jina lake ni BWANA.


Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na muungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo