Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mika 1:2 - Swahili Revised Union Version

2 Sikilizeni, enyi watu wa kabila zote; sikiliza, Ee dunia, na vyote vilivyomo; Bwana MUNGU na ashuhudie juu yenu, yeye Bwana kutoka hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

2 Sikilizeni enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo. Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki, Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

2 Sikilizeni enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo. Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki, Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

2 Sikilizeni enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo. Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki, Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo, ili Bwana Mungu Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

2 Sikieni, enyi mataifa, enyi nyote, sikilizeni, ee dunia na wote mliomo ndani yake, ili bwana Mwenyezi ashuhudie dhidi yenu, Bwana kutoka Hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

2 Sikilizeni, enyi watu wa kabila zote; sikiliza, Ee dunia, na vyote vilivyomo; Bwana MUNGU na ashuhudie juu yenu, yeye Bwana kutoka hekalu lake takatifu.

Tazama sura Nakili




Mika 1:2
33 Marejeleo ya Msalaba  

Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, BWANA hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.


Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, BWANA hakusema kupitia kwangu. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.


BWANA yu katika hekalu lake takatifu. BWANA ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawapima wanadamu.


Nchi na vyote vilivyomo ni mali ya BWANA, Dunia na wote wakaao ndani yake.


Uisikie sauti ya dua yangu nikuombapo, Nikipainulia patakatifu pako mikono yangu.


Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi, Toka maawio ya jua hadi machweo yake.


Kama ningekuwa na njaa singekuambia, Maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.


Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena, Mimi nitakushuhudia, Israeli; Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.


Enyi watu, nawaita ninyi; Na sauti yangu ni kwa wanadamu.


Sikieni, enyi mbingu, tega sikio, Ee nchi, kwa maana BWANA amenena; Nimewalisha watoto na kuwalea, nao wameniasi.


Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.


Maana Bwana MUNGU atanisaidia; kwa sababu hiyo sikutahayari, kwa sababu hiyo nimekaza uso wangu kama jiwe, nami najua ya kuwa sitaona haya.


Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la BWANA.


kwa sababu wametenda upumbavu katika Israeli, nao wamezini na wake za jirani zao, nao wamenena maneno ya uongo kwa jina langu, nisiyowaamuru; nami ndimi nijuaye, nami ni shahidi, asema BWANA.


Wakamwambia Yeremia, BWANA na awe shahidi wa kweli na uaminifu kati yetu; ikiwa hatufanyi sawasawa na neno lile, ambalo BWANA, Mungu wako, atakutuma utuletee.


Sikia, Ee nchi; tazama, nitaleta mabaya juu ya watu hawa, naam, matunda ya mawazo yao, kwa sababu hawakuyasikiliza maneno yangu; tena kwa habari ya sheria yangu, wameikataa.


Roho yangu ilipozimia ndani yangu, Nilimkumbuka BWANA; Maombi yangu yakakufikia, Katika hekalu lako takatifu.


Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo Hujitenga na rehema zao wenyewe.


Lakini BWANA yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.


Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu BWANA amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, ingawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako.


Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami sitasita kutoa ushahidi juu ya wachawi; na juu ya wazinzi, na juu ya waapao kwa uongo; juu ya wamwoneao mwajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema BWANA wa majeshi.


Sikilizeni, enyi mbingu, nami nitanena; Na nchi isikie maneno ya kinywa changu.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa.


Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho anayaambia makanisa.


Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Yeye BWANA atakuwa shahidi kati yetu; hakika yetu tutafanya sawasawa na neno lako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo