Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 8:15 - Swahili Revised Union Version

15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala, watawala huamua yaliyo ya haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala, watawala huamua yaliyo ya haki.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala, watawala huamua yaliyo ya haki.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala na watawala hutunga sheria zilizo za haki,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala na watawala hutunga sheria zilizo za haki,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki.

Tazama sura Nakili




Methali 8:15
27 Marejeleo ya Msalaba  

Na ahimidiwe BWANA, Mungu wako, aliyependezwa nawe, ili akuweke juu ya kiti cha enzi cha Israeli; kwa kuwa BWANA amewapenda Israeli milele, kwa hiyo amekufanya kuwa mfalme, ufanye hukumu na haki.


Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.


Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu watu hawa wako walio wengi?


Ikawa, Hiramu aliposikia maneno yake Sulemani, alifurahi sana, akasema, Na ahimidiwe BWANA leo, aliyempa Daudi mwana mwenye akili juu ya watu hawa walio wengi.


tena katika wana wangu wote (kwani BWANA amenipa wana wengi), amemchagua Sulemani mwanangu ili aketi juu ya kiti cha enzi cha ufalme wa BWANA, juu ya Israeli.


Basi sasa nipe hekima na maarifa, nijue kutoka na kuingia mbele ya watu hawa; kwa kuwa ni nani awezaye kuwatawala watu wako hawa walio wengi?


Naye Mungu akamwambia Sulemani, Kwa sababu neno hili lilikuwamo moyoni mwako, wala hukujitakia mali, wala utajiri, wala utukufu, wala maisha ya wakuchukiao, wala hukujitakia maisha ya siku nyingi; bali umejitakia hekima na maarifa, upate kuwatawala watu wangu, niliokutawaza juu yao;


Na sasa, enyi wafalme, iweni na hekima, Enyi watawala wa dunia, mwaonywa.


Mfalme mkuu upendaye hukumu kwa haki; Umeiimarisha haki; Umefanya hukumu na haki katika Israeli.


Mfalme huithibitisha nchi kwa hukumu; Bali yeye apokeaye rushwa huipindua.


Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia.


nami nitawarejesha tena waamuzi wako kama walivyokuwa hapo kwanza, na washauri wako kama hapo mwanzo; baada ya hayo utaitwa, Mji wa haki, mji mwaminifu.


Katika siku zile, na wakati ule, nitamchipushia Daudi Chipukizi la haki; naye atafanya hukumu na haki katika nchi hii.


Yeye hubadili majira na nyakati; hutengua na kuteua wafalme; huwapa hekima wenye hekima; huwapa wenye ufahamu maarifa;


ya kuwa utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa mwituni, nawe utalazimishwa kula majani kama ng'ombe, nawe utanyeshewa na umande wa mbinguni, na nyakati saba zitapita juu yako; hata utakapojua ya kuwa Aliye Juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye, awaye yote.


Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa mwituni; utalishwa majani kama ng'ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, hata utakapojua ya kuwa Aliye Juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote.


Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.


Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.


Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.


Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA.


BWANA akamwambia Samweli, utamlilia Sauli hadi lini, kwa kuwa mimi nimemkataa asiwatawale Waisraeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakutuma kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.


Hata Samweli alipomwona Sauli, BWANA akamwambia, Huyu ndiye niliyekuambia juu zake; huyu ndiye atakayewamiliki watu wangu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo