Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 6:17 - Swahili Revised Union Version

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Macho ya kiburi, ulimi mdanganyifu, mikono inayoua wasio na hatia,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Macho ya kiburi, ulimi mdanganyifu, mikono inayoua wasio na hatia,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Macho ya kiburi, ulimi mdanganyifu, mikono inayoua wasio na hatia,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia;

Tazama sura Nakili




Methali 6:17
34 Marejeleo ya Msalaba  

Na Manase akazimwaga damu zisizo na hatia, nyingi sana, hata alipokuwa ameijaza Yerusalemu tangu upande huu hata upande huu; zaidi ya kosa lake alilowakosesha Yuda, kutenda yaliyo mabaya machoni pa BWANA.


tena kwa ajili ya damu zisizo na hatia alizozimwaga; kwani aliujaza Yerusalemu damu zisizo na hatia; wala BWANA hakukubali kusamehe.


Mdhalimu kwa kiburi cha uso wake Asema, Mungu Hatapatiliza. Mawazo yake yote ni, Hakuna Mungu;


Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamwangamiza. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitamvumilia.


BWANA, moyo wangu hauna kiburi, Wala macho yangu hayainuki. Wala sijishughulishi na mambo makuu, Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.


Maana Wewe wawaokoa watu wanaoonewa, Na macho ya kiburi utayadhili.


Midomo ya uongo iwe na ububu, Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi, Kwa majivuno na dharau.


Utawaharibu wasemao uongo; BWANA humchukia mwuaji na mwenye hila


Bali mimi, kwa wingi wa fadhili zako, Nitaingia nyumbani mwako; Na kusujudu kwa kicho, Nikilielekea hekalu lako takatifu.


Wakisema, Haya! Njoo pamoja nasi, Na tuvizie ili kumwaga damu; Tumwotee asiye na hatia, bila sababu;


Maana miguu yao huenda mbio maovuni, Nao hufanya haraka ili kumwaga damu.


Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA; Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.


Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.


Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa BWANA; Hakika, hatakosa adhabu.


Maneno mazuri hayapendezi kinywani mwa mpumbavu; Sembuse midomo ya uongo kinywani mwa mkuu.


Mwenye kiburi na moyo wa majivuno, Taa yake ni dhambi.


Ulimi unenao uongo huwachukia wale uliowajeruhi; Na kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.


Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.


Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana.


Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake.


Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.


Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


BWANA akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;


Kuonekana kwa nyuso zao kwashuhudia juu yao, wafunua dhambi yao kama Sodoma, hawaifichi. Ole wa nafsi zao, kwa maana wamejilipa nafsi zao uovu.


Lakini jueni hakika kwamba, mkiniua, mtajiletea juu yenu damu isiyo na hatia itakuwa juu yenu, na juu ya mji huu, na juu ya wenyeji wake; kwa maana ni kweli BWANA amenituma kwenu, kuwaambieni yote mliyoyasikia.


Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa uongo.


isije ikamwagika damu ya asiye makosa kati ya nchi yako akupayo BWANA, Mungu wako, iwe urithi, ikawa na damu juu yako.


Na alaaniwe atwaaye ujira wa kumwua asiye makosa. Na watu wote waseme, Amina.


Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.


Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo