Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 31:22 - Swahili Revised Union Version

22 Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

22 Hujitengenezea matandiko, mavazi yake ni ya zambarau ya kitani safi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

22 Hujitengenezea matandiko, mavazi yake ni ya zambarau ya kitani safi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

22 Hujitengenezea matandiko, mavazi yake ni ya zambarau ya kitani safi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

22 Yeye hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, huvaa kitani safi na urujuani.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

22 Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.

Tazama sura Nakili




Methali 31:22
11 Marejeleo ya Msalaba  

Farao akavua pete yake ya mhuri mkononi mwake, akaitia mkononi mwa Yusufu; akamvika mavazi ya kitani nzuri, na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni mwake.


Ikawa siku ya tatu Esta alijivika mavazi yake ya kifalme, akasimama katika ua wa ndani wa nyumba ya mfalme, kuielekea nyumba ya mfalme; naye mfalme akaketi juu ya kiti chake cha enzi katika nyumba ya mfalme, kuuelekea mlango wa kasri.


Naye Mordekai akatoka usoni pa mfalme, amevaa mavazi ya kifalme, ya rangi ya samawati na nyeupe, mwenye taji kubwa la dhahabu, na joho la kitani safi na rangi ya zambarau. Mji wa Susa wakapaza sauti, wakashangilia.


Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri, Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.


Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.


Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;


Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.


Naye ameruhusiwa kuvikwa kitani nzuri, ing'aayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.


Na uzani wa hizo herini za dhahabu alizozitaka ulipata shekeli za dhahabu elfu moja na mia saba; mbali na makoja na vidani, na mavazi ya rangi ya zambarau waliyokuwa wameyavaa hao wafalme wa Midiani, tena mbali na mikufu iliyokuwa katika shingo za ngamia wao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo