Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 24:16 - Swahili Revised Union Version

16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka, lakini mtu mwovu huangamizwa na janga.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka, lakini mtu mwovu huangamizwa na janga.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 maana mtu mwema huanguka mara nyingi lakini huinuka, lakini mtu mwovu huangamizwa na janga.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena; lakini waovu huangushwa chini na maafa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.

Tazama sura Nakili




Methali 24:16
30 Marejeleo ya Msalaba  

Wakamnywesha tena baba yao mvinyo usiku ule, akaondoka mdogo akalala naye, wala yeye hana habari alipolala wala alipoondoka.


Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.


Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.


Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini BWANA kutoka kwayo yote.


Uovu utamwua asiye haki, Nao wamchukiao mwenye haki watahukumiwa.


Ajapojikwaa hataanguka chini, Maana BWANA humshika mkono na kumtegemeza.


Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.


Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.


Uwalipe jirani zetu mara saba vifuani mwao Laumu zao walizokulaumu, Ee Bwana.


Mjumbe mbaya huanguka maovuni; Bali mjumbe mwaminifu ni afya.


Uovu huwafuatia wenye dhambi; Bali mwenye haki atalipwa mema.


Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake; Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake.


Maana msiba wao utatokea kwa ghafla; Tena ni nani aujuaye uharibifu wa miaka yao.


Basi msiba utampata kwa ghafla; Ghafla atavunjika, bila njia ya kupona.


Nami nitawatawanya mbele ya adui, kama kwa upepo wa mashariki; nami nitaviangalia visogo vyao, wala si nyuso zao, siku ya msiba wao.


Tena utawaambia, BWANA asema hivi, Je! Watu wataanguka, wasisimame tena? Je! Mtu atageuka aende zake, asirudi tena?


Bwana MUNGU asema hivi; Ni jambo baya, jambo baya la namna ya peke yake; angalia, linakuja.


Bikira wa Israeli ameanguka; hatainuka tena; Ameangushwa katika nchi yake; hakuna mtu wa kumwinua.


Na hao waapao kwa dhambi ya Samaria, na kusema, Kama aishivyo Mungu wako, Ee Dani, na, Kama iishivyo njia ya Beer-sheba, hao nao wataanguka, wasiinuke tena.


Lakini kama hamtaki kufanya neno hilo, ninyi mmefanya dhambi mbele za BWANA, nanyi jueni ya kwamba hiyo dhambi yenu itawapata, hapana budi.


Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na wadudu, akatokwa na roho.


Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla, kama vile uchungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.


Daudi akasema, Aishivyo BWANA, BWANA atampiga; au siku yake ya kufa itampata; atashuka kwenda vitani na kupotea.


Ndipo Sauli akamwambia yule mchukua silaha zake, Futa upanga wako, unichome nao; wasije watu hawa wasiotahiriwa wakanichoma, na kunisimanga. Lakini huyo mchukua silaha zake akakataa; kwa sababu aliogopa sana. Basi Sauli akautwaa upanga wake, akauangukia.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo