Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 18:10 - Swahili Revised Union Version

10 Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Jina la Mwenyezi-Mungu ni mnara imara; mwadilifu huukimbilia akawa salama.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Jina la Mwenyezi-Mungu ni mnara imara; mwadilifu huukimbilia akawa salama.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Jina la Mwenyezi-Mungu ni mnara imara; mwadilifu huukimbilia akawa salama.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Jina la Mwenyezi Mungu ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Jina la bwana ni ngome imara, wenye haki huikimbilia na kuwa salama.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

10 Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.

Tazama sura Nakili




Methali 18:10
29 Marejeleo ya Msalaba  

Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na tisa, BWANA akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu.


Uniokoe sasa kutoka kwa mkono wa ndugu yangu, mkono wa Esau, maana mimi ninamwogopa, asije akaniua, na kina mama pamoja na watoto.


akasema, BWANA ndiye jabali langu, na ngome yangu, na mwokozi wangu,


Mungu wa mwamba wangu, nitamwamini yeye; Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, mnara wangu, na kimbilio langu; Mwokozi wangu, waniokoa na jeuri.


Yeye ni mnara wa wokovu kwa mfalme wake; Amfanyia fadhili masihi wake, Kwa Daudi na wazawa wake, hata milele.


Mwamba wangu na ngome yangu, Nguzo yangu na mwokozi wangu Ngao yangu ninayemkimbilia, Huwatiisha watu wangu chini yangu.


BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.


Akutumie msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni.


BWANA ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani?


Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.


Atasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.


nami nilimtokea Abrahamu, na Isaka, na Yakobo, kama Mungu Mwenyezi, bali kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.


Kumcha BWANA ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio.


Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye BWANA atakuwa salama.


Mtumainini BWANA siku zote Maana BWANA YEHOVA ni mwamba wa milele.


Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.


Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto wa kiume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.


Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, BWANA ni haki yetu.


MUNGU, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.


Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.


Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.


Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la BWANA wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.


Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo