Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 17:17 - Swahili Revised Union Version

17 Rafiki hupenda sikuzote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote, ndugu huzaliwa asaidie wakati wa taabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote, ndugu huzaliwa asaidie wakati wa taabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote, ndugu huzaliwa asaidie wakati wa taabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

17 Rafiki hupenda siku zote; Na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu.

Tazama sura Nakili




Methali 17:17
16 Marejeleo ya Msalaba  

Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani, ndugu yangu, Ulikuwa ukinipendeza sana; Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, Kupita upendo wa wanawake.


Naye Itai akamjibu mfalme akasema, Kama aishivyo BWANA, na bwana wangu mfalme aishivyo, hakika yake kila mahali atakapokuwapo mfalme, bwana wangu, ikiwa ni kwa kufa au ikiwa ni kwa kuishi, ndipo atakapokuwapo na mtumishi wako.


Kwa maana wewe ukinyamaza kabisa wakati huu, ndipo kutakapowatokea Wayahudi msaada na wokovu kwa njia nyingine; ila wewe utaangamia pamoja na mlango wote wa baba yako; lakini ni nani ajuaye kama wewe hukuujia ufalme kwa ajili ya wakati kama huu?


Mtu mshupavu huleta fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.


Ajifanyiaye marafiki wengi ni kwa maangamizi yake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.


Mwana mpumbavu ni msiba kwa babaye; Na ugomvi wa mke kama kudondoka kwa matone daima.


Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.


Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii haoni haya kuwaita ndugu zake;


Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirudi nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu;


Nao Yonathani na Daudi wakaahidiana, kwa kuwa alimpenda kama roho yake mwenyewe.


Lakini huyo Yonathani, mwana wake Sauli, alikuwa akipendezwa sana na Daudi. Basi Yonathani akamwambia Daudi, akasema, Sauli, baba yangu, anakusudia kukuua; basi, nakusihi, ujiangalie sana asubuhi, ukae mahali pa siri na kujificha;


na mimi nitatoka nje na kusimama kando ya babangu huko shambani ulipo wewe, nami nitazungumza na babangu habari zako; nami nikiona neno lolote nitakuambia.


Naye Yonathani akamwapisha Daudi mara ya pili, kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake; kwa maana alimpenda kama alivyoipenda roho yake mwenyewe.


Ndipo Yonathani, mwana wa Sauli, akainuka akamwendea Daudi huko Horeshi, akamtia nguvu mkono wake katika Mungu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo