Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 14:18 - Swahili Revised Union Version

18 Wajinga hurithi upumbavu; Bali wenye busara huvikwa taji la maarifa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini wenye busara hutuzwa taji ya maarifa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini wenye busara hutuzwa taji ya maarifa.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

18 Wajinga hurithi upumbavu, lakini wenye busara hutuzwa taji ya maarifa.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

18 Mjinga hurithi upumbavu, bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

18 Mjinga hurithi upumbavu, bali wenye busara huvikwa maarifa kichwani kama taji.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

18 Wajinga hurithi upumbavu; Bali wenye busara huvikwa taji la maarifa.

Tazama sura Nakili




Methali 14:18
12 Marejeleo ya Msalaba  

Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.


Wabaya huinama mbele ya wema, Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.


Wenye hekima wataurithi utukufu, Bali kukuzwa kwa wapumbavu ni fedheha.


Ee BWANA, nguvu zangu, ngome yangu, na kimbilio langu siku ya taabu, kwako wewe watakuja mataifa yote toka ncha za dunia, wakisema, Baba zenu hawakurithi kitu ila uongo, naam, ubatili na vitu visivyofaa.


Lakini bila shaka tutalitimiza kila neno lililotoka katika vinywa vyetu, kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, kama tulivyotenda sisi, na baba zetu, na wafalme wetu, na wakuu wetu, katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu; maana wakati huo tulikuwa na chakula tele, na kufanikiwa, wala hatukuona mabaya.


Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.


baada ya hayo nimewekewa taji la haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.


Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu;


Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtalipokea taji la utukufu, lile lisilokauka.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo