Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Methali 10:14 - Swahili Revised Union Version

14 Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, lakini kuropoka kwa mpumbavu huleta maangamizi haraka.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, lakini kuropoka kwa mpumbavu huleta maangamizi haraka.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, lakini kuropoka kwa mpumbavu huleta maangamizi haraka.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

14 Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

14 Watu wenye akili huweka akiba ya maarifa; Bali kinywa cha mpumbavu ni uangamivu ulio karibu.

Tazama sura Nakili




Methali 10:14
17 Marejeleo ya Msalaba  

mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.


Akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.


Aliye na akili moyoni mwake atapokea agizo; Bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataanguka.


Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa; Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.


Yeye alindaye kinywa chake huilinda nafsi yake; Bali afunuaye midomo yake atapata uharibifu.


Mtu mwenye moyo wa ukaidi hatapata mema; Na mwenye ulimi wa upotovu huanguka katika misiba.


Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.


Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.


Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.


Apataye hekima hujipenda nafsi yake; Ashikaye ufahamu atapata mema.


Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.


Mwelimishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima; Mfundishe mwenye haki, naye atazidi kuwa na elimu;


Maneno ya kinywa chake mwenye hekima yana neema; Bali midomo ya mpumbavu itammeza nafsi yake.


Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.


Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile.


Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo