Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Mathayo 14:20 - Swahili Revised Union Version

20 Wakala wote wakashiba; wakayaokota mabaki ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili, vimejaa.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

20 Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

20 Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

20 Watu wote wakala, wakashiba. Kisha wanafunzi wakakusanya mabaki, wakajaza vikapu kumi na viwili.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

20 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

20 Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

20 Wakala wote wakashiba; wakayaokota mabaki ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili, vimejaa.

Tazama sura Nakili




Mathayo 14:20
21 Marejeleo ya Msalaba  

Nimeyasikia manung'uniko ya wana wa Israeli; haya sema nao ukinena, Wakati wa jioni mtakula nyama, na wakati wa asubuhi mtashiba mkate; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Musa akasema, Ndilo litakalokuwa, hapo BWANA atakapowapa nyama wakati wa jioni mle, na asubuhi mikate hata mkakinai; kwa kuwa BWANA asikia manung'uniko yenu mliyomnung'unikia yeye; na sisi tu nani? Manung'uniko yenu hayakuwa juu yetu sisi, ila juu ya BWANA.


Mwenye haki hula akaishibisha nafsi yake; Bali tumbo la mtu mbaya litaona njaa.


Hapo nitakapovunja tegemeo lenu la mkate, wanawake kumi wataoka mikate yenu katika tanuri moja, nao watawapa mikate yenu tena kwa kupima kwa mizani; nanyi mtakula, lakini hamtashiba.


Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamtosheki na vinywaji; mnajivika nguo lakini hampati joto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotobokatoboka.


Nao waliokula walikuwa wanaume wapatao elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto.


Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?


Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.


Wenye njaa amewashibisha mema, Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.


Wakala, wakashiba wote; na katika vile vipande vilivyowabakia walikusanya vikapu kumi na viwili.


Filipo akamjibu, Mikate ya dinari mia mbili haiwatoshi, kila mmoja apate kidogo tu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo