Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Maombolezo 5:6 - Swahili Revised Union Version

6 Tumewapa hao Wamisri mkono; Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

6 Wamisri na Waashuru tumewanyoshea mikono, ili tupate chakula cha kutosha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

6 Wamisri na Waashuru tumewanyoshea mikono, ili tupate chakula cha kutosha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

6 Wamisri na Waashuru tumewanyoshea mikono, ili tupate chakula cha kutosha.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

6 Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

6 Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

6 Tumewapa hao Wamisri mkono; Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.

Tazama sura Nakili




Maombolezo 5:6
15 Marejeleo ya Msalaba  

Abrahamu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu,


Alipotoka huko akamkuta Yehonadabu mwana wa Rekabu akija kumlaki; akamsalimu akamwambia, Je! Moyo wako umenyoka, kama moyo wangu ulivyo pamoja na moyo wako? Akajibu Yehonadabu, Ndio. Yehu akamwambia, Kama ndio, nipe mkono wako. Akampa mkono, akamkalisha pamoja naye garini.


Ulimwendea mfalme na mafuta ya marhamu, ukaongeza manukato yako, ukawatuma wajumbe wako waende mbali, ukajidhili sana hadi kuzimu.


Na sasa una nini utakayofaidi katika njia iendayo Misri, kunywa maji ya Shihori? Au una nini utakayofaidi katika njia iendayo Ashuru, kunywa maji ya ule Mto?


Mbona unatangatanga hivi upate kugeuza mwendo wako? Utaona haya kwa ajili ya Misri pia, kama ulivyoona haya kwa ajili ya Ashuru.


Mpigieni kelele pande zote; amejitoa; Maboma yake yameanguka, kuta zake zimebomolewa; Kwa maana ni kisasi cha BWANA; mlipizeni kisasi; Kama yeye alivyotenda, mtendeni yeye.


Macho yetu yamechoka Kwa kuutazamia bure msaada wetu; Katika kungoja kwetu tumengojea taifa Lisiloweza kutuokoa.


Kwa maana amekidharau kiapo kwa kulivunja agano; na tazama, ametia mkono wake, na pamoja na hayo ameyatenda mambo hayo yote; hataokoka.


Efraimu hujilisha upepo, na kuandamana na upepo wa mashariki; haachi kuongeza uongo na uharibifu; nao wafanya agano na Ashuru, na mafuta huchukuliwa kwenda Misri.


Efraimu alipouona ugonjwa wake, na Yuda jeraha lake, ndipo Efraimu alipokwenda kwa Ashuru, akatuma watu kwa mfalme Yarebu; lakini yeye hawezi kuwapoza, wala hatawaponya jeraha lenu.


Naye Efraimu amekuwa kama njiwa mpumbavu, asiye na fahamu; humwita Misri, huenda Ashuru.


Hawatakaa katika nchi ya BWANA; lakini Efraimu atarudi Misri, nao watakula chakula najisi katika Ashuru.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo