Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Samueli 19:1 - Swahili Revised Union Version

1 Kisha Yoabu akaambiwa, Angalia, mfalme anamlilia Absalomu na kumwombolezea.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Yoabu aliambiwa kwamba mfalme alikuwa akilia na kuomboleza juu ya kifo cha Absalomu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Yoabu aliambiwa kwamba mfalme alikuwa akilia na kuomboleza juu ya kifo cha Absalomu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Yoabu aliambiwa kwamba mfalme alikuwa akilia na kuomboleza juu ya kifo cha Absalomu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Yoabu akaambiwa, “Mfalme analia na kumwombolezea Absalomu.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 Yoabu akaambiwa, “Mfalme analia na kumwombolezea Absalomu.”

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 Kisha Yoabu akaambiwa, Angalia, mfalme anamlilia Absalomu na kumwombolezea.

Tazama sura Nakili




2 Samueli 19:1
9 Marejeleo ya Msalaba  

Wanawe wote, na binti zake wote, wakaondoka wamtulize, lakini akakataa kutulizwa, akasema, La! Nitashuka kaburini kwa mwanangu, nikiomboleza. Basi baba yake akamlilia.


Yule mtu akamwambia Yoabu, Kama ningalipata fedha elfu moja mkononi mwangu, hata hivyo singalinyosha mkono wangu juu ya mwana wa mfalme; kwa maana mfalme masikioni mwetu alikuagiza wewe, na Abishai na Itai, akisema, Angalieni sana mtu yeyote yule asimguse yule kijana, Absalomu.


Ndipo Yoabu akasema, Siwezi kungoja na kusema nawe hivi. Akachukua mikuki mitatu midogo mkononi mwake, akamchoma Absalomu moyoni, alipokuwa bado hai katikati ya ule mwaloni.


Yoabu akamwambia, Wewe hutakuwa mchukua habari leo, siku nyingine utachukua habari; lakini leo hutachukua habari, kwa sababu mwana wa mfalme amekufa.


Naye mfalme akataabika sana, akapanda juu, akaingia kile chumba kilichokuwa juu ya lango, akalia; na katika kwenda kwake alisema hivi, Mwanangu Absalomu! Ee mwanangu! Mwanangu Absalomu! Laiti ningalikufa badala yako, Absalomu, mwanangu, mwanangu!


Mfalme akawaamuru Yoabu na Abishai na Itai, akasema, Mtendeeni yule kijana, Absalomu, kwa upole kwa ajili yangu. Nao watu wote wakasikia, mfalme alipowaagiza makamanda wote kuhusu Absalomu.


Na kushinda kwao vitani siku ile kukageuzwa kuwa maombolezo kwa watu wote; maana watu walisikia siku ile ya kwamba, Mfalme anahuzunika kwa ajili ya mwanawe.


Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye, Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.


Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimdunga; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo