Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




1 Timotheo 2:4 - Swahili Revised Union Version

4 ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

4 ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

4 ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

4 ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

4 anayetaka watu wote waokolewe na wafikie kuijua kweli.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

4 ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.

Tazama sura Nakili




1 Timotheo 2:4
32 Marejeleo ya Msalaba  

Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.


naam, asema hivi, Ni neno dogo sana wewe kuwa mtumishi wangu ili kuyainua makabila ya Yakobo, na kuwarejesha watu wa Israeli waliohifadhiwa; zaidi ya hayo nitakutoa uwe nuru ya mataifa, upate kuwa wokovu wangu hata miisho ya dunia.


Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.


Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila gharama.


Je! Mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? Asema Bwana MUNGU; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?


Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye, asema Bwana MUNGU; basi ghairini, mkaishi.


Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sikufurahii kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?


Kwa maana dunia itajazwa maarifa ya utukufu wa BWANA, kama maji yaifunikavyo bahari.


Basi, nendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;


Akawaambia, Nendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.


Uwajulishe watu wake wokovu, Kwa kusamehewa dhambi zao.


Bwana akamwambia mtumwa, Toka nje uende barabarani na mipakani, ukawashurutishe kuingia ndani, nyumba yangu ipate kujaa.


na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu.


Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.


Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.


Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.


nipate kuwatia wivu walio damu moja na mimi na kuwaokoa baadhi yao.


kwa maana twajitaabisha na kujitahidi kwa kusudi hili, kwa sababu tunamtumaini Mungu aliye hai, aliye Mwokozi wa watu wote, hasa wa wale waaminio.


akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awajalie ili watubu na kuijua kweli;


wakijifunza siku zote, ila wasiweze kabisa kuufikia ujuzi wa kweli.


Paulo, mtumwa wa Mungu, na mtume wa Yesu Kristo; kwa ajili ya imani ya wateule wa Mungu, na ujuzi wa kweli ile iletayo utauwa;


Maana neema ya Mungu iwaokoao wanadamu wote imefunuliwa;


Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;


Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli.


Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyodhani anakawia, bali huwavumilia, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote wafikie toba.


Mzee, kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli; wala si mimi peke yangu, bali na wote waijuayo ile kweli;


Kisha nikaona malaika mwingine, akiruka katikati ya mbingu, akiwa na Injili ya milele, awahubirie hao wakaao juu ya nchi, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo