Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zekaria 4:1 - Swahili Revised Union Version

Na yule malaika aliyesema nami akanijia mara ya pili, akaniamsha, kama mtu aamshwavyo katika usingizi wake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yule malaika aliyeongea nami, akanijia tena, akaniamsha kama kumwamsha mtu usingizini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yule malaika aliyeongea nami, akanijia tena, akaniamsha kama kumwamsha mtu usingizini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yule malaika aliyeongea nami, akanijia tena, akaniamsha kama kumwamsha mtu usingizini.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kisha malaika aliyezungumza nami akarudi na kuniamsha, kama mtu aamshwavyo kutoka usingizini.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kisha malaika aliyezungumza nami akarudi na kuniamsha, kama mtu aamshwavyo kutoka usingizi wake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na yule malaika aliyesema nami akanijia mara ya pili, akaniamsha, kama mtu aamshwavyo katika usingizi wake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zekaria 4:1
12 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, nikaamka, nikaangalia; na usingizi wangu ulikuwa mtamu kwangu.


Basi alipokuwa akisema nami, nilishikwa na usingizi mzito na uso wangu uliielekea nchi; lakini alinigusa, akanisimamisha wima.


Naye BWANA akamjibu yule malaika aliyesema nami kwa maneno mazuri, maneno yenye faraja.


Nami nikamwuliza yule malaika aliyesema nami, Nini hizi? Naye akanijibu, Hizi ndizo pembe zilizowatawanya watu wa Yuda, na Israeli, na Yerusalemu.


Ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, ni nini hawa? Basi yule malaika aliyesema nami akaniambia, Nitakuonesha ni nini hawa.


Na tazama, yule malaika aliyesema nami akasimama karibu, na malaika mwingine akatoka ili kuonana naye;


Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.


Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi; lakini walipokwisha amka waliuona utukufu wake, na wale wawili waliosimama pamoja naye.