Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 3:33 - Swahili Revised Union Version

Yeye aliyeukubali ushuhuda wake ametia mhuri ya kwamba Mungu ni kweli.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lakini mtu yeyote anayekubali ujumbe wake anathibitisha kwamba Mungu ni kweli.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba Mwenyezi Mungu ni kweli.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye aliyeukubali ushuhuda wake ametia mhuri ya kwamba Mungu ni kweli.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 3:33
17 Marejeleo ya Msalaba  

Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa mhuri na Baba, yaani, Mungu.


Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenituma ni kweli, nami niliyoyasikia kwake, ndiyo ninenayo katika ulimwengu.


Basi nikiisha kuimaliza kazi hiyo, na kuwatilia mhuri tunda hilo, nitapitia kwenu, kwenda Spania.


Naye aliipokea dalili hii ya kutahiriwa, mhuri wa ile haki ya imani aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa; apate kuwa baba yao wote waaminio, ijapokuwa hawakutahiriwa, ili na wao pia wahesabiwe haki;


Kwa maana ikiwa mimi si mtume kwa wengine, lakini ni mtume kwenu ninyi; kwa maana ninyi ndinyi mhuri wa utume wangu katika Bwana.


Lakini kama Mungu alivyo mwaminifu, neno letu kwenu si Ndiyo na Siyo.


naye ndiye aliyetutia mhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu.


Nanyi pia katika huyo mmekwisha kulisikia neno la kweli, Habari Njema za wokovu wenu; tena mmekwisha kumwamini yeye, na kutiwa mhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu.


Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa mhuri hata siku ya ukombozi.


Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye mhuri huu, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila aliitaye jina la Bwana na auache uovu.


Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;


Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, tunamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo ndani yetu.