Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 18:4 - Swahili Revised Union Version

Basi Yesu, huku akijua yote yatakayompata, akatokea, akawaambia, Ni nani mnayemtafuta?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawauliza, “Mnamtafuta nani?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawauliza, “Mnamtafuta nani?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawauliza, “Mnamtafuta nani?”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Isa, akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao, akawauliza, “Mnamtafuta nani?”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Isa akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Basi Yesu, huku akijua yote yatakayompata, akatokea, akawaambia, Ni nani mnayemtafuta?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 18:4
27 Marejeleo ya Msalaba  

Kama BWANA, Mungu wako, aishivyo, hakuna taifa wala ufalme ambao bwana wangu hakutuma watu wakutafute; na waliposema, Hayupo, akawaapisha ule ufalme, na taifa, ya kwamba hawakukuona.


Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia.


Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumainia BWANA.


Sitayaogopa maelfu na maelfu ya watu, Waliojipanga Juu yangu pande zote.


Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba.


Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.


Mnajua ya kuwa baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, na Mwana wa Adamu atasalitiwa asulubiwe.


Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti.


Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.


Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa ningali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika vitabu vya Manabii na Zaburi.


Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, huku akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye akiwa amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo.


Kwa maana alimjua yeye atakayemsaliti; ndiyo maana alisema, Si nyote mlio safi.


Wao wakamjibu, Ni Yesu Mnazareti. Yesu akawaambia, Ni mimi. Yuda naye aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.


Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti.


Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.


Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti.


Umenijulisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako.


Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.