Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yohana 10:20 - Swahili Revised Union Version

Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wengi wao wakasema, “Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wengi wao wakasema, “Huyu amepagawa na pepo mchafu, naye amechanganyikiwa.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yohana 10:20
15 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani angeyajali? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.


BWANA amekufanya kuhani badala ya Yehoyada, kuhani, ili mpate kuwa watumishi katika nyumba ya BWANA, kwa kila mtu aliye na wazimu, na kwa kila mtu ajifanyaye kuwa nabii, umtie katika mkatale na pingu.


Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli, je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake?


Maana Yohana alikuja, hali wala hanywi, wakasema, Ana pepo.


Lakini Mafarisayo wakasema, Kwa nguvu za mkuu wa pepo atoa pepo.


Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili.


Mkutano wakajibu, Ama! Una pepo! Ni nani anayetafuta kukuua?


Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng'amua ya kuwa una pepo. Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.


Alipokuwa akijitetea hivi, Festo akasema kwa sauti kuu, Paulo, una wazimu, kusoma kwako kwingi kumekugeuza akili.