Waebrania 3:11 - Swahili Revised Union Version Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Basi, nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’ Biblia Habari Njema - BHND Basi, nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’ Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Basi, nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’” Neno: Bibilia Takatifu Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’” Neno: Maandiko Matakatifu Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, ‘Kamwe hawataingia rahani mwangu.’ ” BIBLIA KISWAHILI Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu. |
Basi Mwamaleki na Mkanaani wakaa katika bonde; kesho geukeni, mkaende jangwani kwa njia iendayo Bahari ya Shamu.
Mimi BWANA nimekwisha nena, hakika yangu ndilo nitakaloutenda mkutano mwovu huu wote, waliokusanyika juu yangu; wataangamia katika nyika hii, nako ndiko watakakokufa.
Na siku tulizokuwa tukienda kutoka Kadesh-barnea hata tulipovuka kijito cha Zeredi, ilikuwa ni miaka thelathini na minane; maana, hata walipokwisha kuangamizwa watu wa vita kutoka kati ya kambi, kizazi chao chote, kama walivyoapiwa na BWANA.
Maana sisi tulioamini tunaingia katika pumziko lile; kama vile alivyosema, Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia pumzikoni mwangu: ijapokuwa zile kazi zilimalizika tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu.