Obadia 1:8 - Swahili Revised Union Version Siku hiyo, je! Sitawaangamiza watu wenye akili katika Edomu, na wenye ufahamu katika kilima cha Esau? Asema BWANA. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Mimi Mwenyezi-Mungu nakuuliza hivi: Je, siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu na wenye maarifa kutoka mlima Esau? Biblia Habari Njema - BHND Mimi Mwenyezi-Mungu nakuuliza hivi: Je, siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu na wenye maarifa kutoka mlima Esau? Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Mimi Mwenyezi-Mungu nakuuliza hivi: je, siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu na wenye maarifa kutoka mlima Esau? Neno: Bibilia Takatifu “Katika siku hiyo,” asema Mwenyezi Mungu, “je, sitaangamiza wenye hekima wa Edomu, hao wenye ufahamu katika milima ya Esau? Neno: Maandiko Matakatifu “Katika siku hiyo,” asema bwana, “je, sitaangamiza watu wenye hekima wa Edomu, watu wenye ufahamu katika milima ya Esau? BIBLIA KISWAHILI Siku hiyo, je! Sitawaangamiza watu wenye akili katika Edomu, na wenye ufahamu katika kilima cha Esau? Asema BWANA. |
Wakuu wa Soani wamekuwa wapumbavu kabisa; washauri wenye hekima wa Farao, ushauri wao umepumbazika; mwawezaje kumwambia Farao, Mimi ni mwana wa wenye hekima, ni mwana wa wafalme wa zamani?
Wako wapi, basi, watu wako wenye hekima? Na wakuambie sasa; na wajue mambo aliyokusudia BWANA wa majeshi juu ya Misri.
Na roho yao Misri itaondolewa, nami nitaiharibu mipango yao, nao watakwenda kwa sanamu zao, na kwa waganga, na kwa wapiga ramli na kwa wachawi.
kwa sababu hiyo mimi nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, kazi ya ajabu na mwujiza; na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa.