Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mwanzo 1:25 - Swahili Revised Union Version

Mungu akaumba aina zote za wanyama wa porini na wa kufugwa na viumbe vyote vitambaavyo nchini; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mungu akafanya wanyama pori kulingana na aina zake, mifugo kulingana na aina zake, na viumbe vyote vinavyotambaa ardhini kulingana na aina zake. Mungu akaona kuwa hili ni jema.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mwenyezi Mungu akafanya wanyama pori kulingana na aina zake, wanyama wa kufugwa kulingana na aina zake, na viumbe vyote vitambaavyo juu ya ardhi kulingana na aina zake. Mwenyezi Mungu akaona kuwa hili ni jema.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mungu akaumba aina zote za wanyama wa porini na wa kufugwa na viumbe vyote vitambaavyo juu ya nchi; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mwanzo 1:25
9 Marejeleo ya Msalaba  

Wakafa watu wote waendao juu ya nchi, na ndege, na wanyama wa kufugwa, na kila mnyama wa mwitu, na kila kitambaacho chenye kutambaa juu ya nchi, na kila mwanadamu;


kila kitu chenye pumzi ya roho ya uhai puani mwake kikafa, kila kilichokuwako katika nchi kavu.


Lakini sasa waulize hao wanyama, nao watakufundisha; Na ndege wa angani, nao watakuambia;


Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake; Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.


Sitanyamaa kusema habari za via vyake, Wala nguvu zake kuu, wala umbo lake zuri.


Mimi nimeiumba dunia hii, wanadamu na wanyama walio katika nchi, kwa uweza wangu mkuu, na kwa mkono wangu ulionyoshwa; nami nawapa watu kama inipendezavyo.


kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba.