Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 26:21 - Swahili Revised Union Version

Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, Na kama kuni juu ya moto; Ndivyo mtu mgomvi achocheavyo uadui.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kama vile makaa au kuni huchochea moto, ndivyo mgomvi achocheavyo ugomvi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kama vile makaa au kuni huchochea moto, ndivyo mgomvi achocheavyo ugomvi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kama vile makaa au kuni huchochea moto, ndivyo mgomvi achocheavyo ugomvi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, Na kama kuni juu ya moto; Ndivyo mtu mgomvi achocheavyo uadui.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 26:21
8 Marejeleo ya Msalaba  

Basi ilitukia ya kwamba kulikuwapo mtu asiyefaa, jina lake akiitwa Sheba, mwana wa Bikri, Mbenyamini; naye akapiga tarumbeta, akasema, Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese; nendeni kila mtu hemani kwake, enyi Israeli.


Ikawa, Israeli wote waliposikia ya kwamba Yeroboamu amerudi, wakapeleka watu wakamwita aje mkutanoni, wakamfanya mfalme juu ya Israeli wote; wala hapakuwa na mtu aliyeshikamana na nyumba ya Daudi, ila kabila la Yuda peke yake.


Mishale ya mtu hodari iliyochongoka, Pamoja na makaa ya mretemu.


Kuchukiana huleta fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.


Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.


Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.


Kwa maana kupiga maziwa huleta siagi; Na kupiga pua hutokeza damu; kadhalika kuchochea hasira hutokeza ugomvi.