Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 2:21 - Swahili Revised Union Version

Maana wanyofu watakaa katika nchi, Na wakamilifu watadumu ndani yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Maana wanyofu wataipata nchi, na waaminifu watadumu ndani yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Maana wanyofu wataipata nchi, na waaminifu watadumu ndani yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Maana wanyofu wataipata nchi, na waaminifu watadumu ndani yake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa maana wanyofu wataishi katika nchi, nao wasio na lawama watabakia ndani yake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana wanyofu watakaa katika nchi, Na wakamilifu watadumu ndani yake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 2:21
12 Marejeleo ya Msalaba  

Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.


Basi hivyo BWANA akaubariki huo mwisho wa Ayubu zaidi ya mwanzo wake; naye alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, na ngamia elfu sita, na jozi za ng'ombe elfu moja, na punda wake elfu moja.


Bali wenye upole watairithi nchi, Watajifurahisha kwa wingi wa amani.


BWANA huwatunza waaminifu, Na urithi wao utakuwa wa milele.


Maana waliobarikiwa na BWANA watairithi nchi, Nao waliolaaniwa naye watakatiliwa mbali.


Wenye haki watairithi nchi, Nao watakaa humo milele.


Umtumaini BWANA ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.


Maana watenda mabaya watakatiliwa mbali, Bali wamngojao BWANA ndio watakaoirithi nchi.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Mwenye haki hataondolewa milele; Bali wasio haki hawatakaa katika nchi.


Kila mtu awapotezaye wenye haki katika njia mbaya, Ataanguka katika rima lake mwenyewe; Bali wakamilifu watarithi mema.