Methali 19:9 - Swahili Revised Union Version Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa; asemaye uongo ataangamia. Biblia Habari Njema - BHND Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa; asemaye uongo ataangamia. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa; asemaye uongo ataangamia. Neno: Bibilia Takatifu Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo ataangamia. Neno: Maandiko Matakatifu Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo ataangamia. BIBLIA KISWAHILI Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia. |
Kwa kuwa ninyi mmemhuzunisha moyo mwenye haki kwa uongo, ambaye mimi sikumhuzunisha; na kuitia nguvu mikono ya mtu mbaya, hata asigeuke, na kuiacha njia yake mbaya, na kuhifadhika;
Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki Danieli, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao, na wake zao; na wale simba wakawashinda wakaivunja mifupa yao vipande vipande, kabla hawajafika chini ya tundu.
Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao hao walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wakiwa hai katika lile ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;
Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.
Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya.