Methali 1:6 - Swahili Revised Union Version Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao. Biblia Habari Njema - BHND Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Mtu aelewe methali na mifano, maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao. Neno: Bibilia Takatifu kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima. Neno: Maandiko Matakatifu kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima. BIBLIA KISWAHILI Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao. |
Maneno yao wenye hekima huwa mfano wa michokoo; na kama misumari iliyogongomewa sana; ndivyo yalivyo maneno yao walio wakuu wa makusanyiko, ambayo yatoka kwa mchungaji mmoja.
Na wakati wa mwisho wa ufalme wao, wakosaji watakapotimia kilele cha uovu wao, mfalme mwenye uso mkali, afahamuye mafumbo, atasimama.
Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumteta mtumishi wangu, huyo Musa?
Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje, yote hufanywa kwa mifano,
wala pasipo mfano hakusema nao; lakini akawaeleza wanafunzi wake mwenyewe mambo yote kwa faragha.
Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoeshwa kupambanua mema na mabaya.
akisema juu ya mambo haya kama afanyavyo katika barua zake zote pia, katika barua hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuyaelewa na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wapotoavyo Maandiko mengine, na kujiletea maangamizi wao wenyewe.