Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 27:5 - Swahili Revised Union Version

Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Naye akazitupa zile fedha hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Naye akazitupa zile fedha hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Naye akazitupa zile fedha hekaluni, akatoka nje, akaenda akajinyonga.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi Yuda akavitupa vile vipande vya fedha ndani ya Hekalu akaondoka akaenda kujinyonga.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 27:5
12 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Ahithofeli alipoona ya kuwa ushauri wake haukufuatwa, akatandika punda wake, akaondoka, akaenda nyumbani kwake, mjini mwake, akaitengeneza nyumba yake, akajinyonga; akafa, akazikwa kaburini mwa babaye.


Ikawa Zimri alipoona ya kuwa mji umetwaliwa, akaingia ngomeni mwa nyumba ya mfalme, akaiteketeza nyumba ya mfalme juu yake kwa moto, akafa;


Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Mkufuru Mungu, ufe.


Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa, Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.


Nawe, Ee Mungu, utawateremsha, Wafikie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.


Na baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.


Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni fedha ya damu.


Na wale watu walikuwa wakimngojea Zakaria, wakastaajabia kukawia kwake mle hekaluni.


kama ilivyokuwa desturi ya ukuhani, kura ilimwangukia kuingia katika hekalu la Bwana ili kufukiza uvumba.


Ndipo akamwita kwa haraka huyo kijana aliyekuwa anamchukulia silaha zake, na kumwambia, Futa upanga wako, uniue, ili watu wasiseme juu yangu, Aliuawa na mwanamke. Basi huyo kijana wake akamchoma upanga, naye akafa.