Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Matendo 21:9 - Swahili Revised Union Version

Mtu huyu alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Alikuwa na binti wanne ambao walikuwa na kipaji cha unabii.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Alikuwa na binti wanne ambao walikuwa na kipaji cha unabii.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Alikuwa na binti wanne ambao walikuwa na kipaji cha unabii.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Filipo alikuwa na binti wanne mabikira waliokuwa wanatoa unabii.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Filipo alikuwa na binti wanne mabikira waliokuwa wanatoa unabii.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mtu huyu alikuwa na binti wanne, mabikira, waliokuwa wakitabiri.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Matendo 21:9
13 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Hilkia kuhani, na Ahikamu, na Akbori, na Shafani, na Asaya, wakamwendea Hulda, nabii wa kike, mkewe Shalumu, mwana wa Tikva, mwana wa Harhasi, mtunza mavazi ya mfalme; (naye alikaa Yerusalemu katika mtaa wa pili;) wakasema naye.


Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, Tobia na Sanbalati kulingana na hayo matendo yao, na yule nabii mwanamke Noadia.


Na Miriamu, nabii mwanamke, dada yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza.


Na wewe, mwanadamu, kaza uso wako juu ya binti za watu wako, watabirio kwa akili zao wenyewe; ukatabiri juu yao,


Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, wa kiume na wa kike, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;


Palikuwa na nabii mwanamke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.


Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kulelewa wa mfalme Herode, na Sauli.


Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.


Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema.


Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu.


Basi Debora, nabii mwanamke, mkewe Lapidothi, ndiye aliyekuwa mwamuzi wa Israeli wakati ule.