Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 3:59 - Swahili Revised Union Version

Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee BWANA; Unihukumie neno langu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu, uniamulie kwa wema kisa changu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu, uniamulie kwa wema kisa changu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Umeuona uovu niliotendewa ee Mwenyezi-Mungu, uniamulie kwa wema kisa changu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Umeona, Ee Mwenyezi Mungu, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Umeona, Ee bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee BWANA; Unihukumie neno langu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 3:59
16 Marejeleo ya Msalaba  

Raheli akasema, Mungu amenipa haki yangu, naye amesikia sauti yangu, akanipa mwana. Kwa hiyo akamwita jina lake Dani.


Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu.


Umeona, maana unaangalia matatizo na dhiki, Uyatwae mkononi mwako. Mtu duni hukuachia nafsi yake, Maana umekuwa msaidizi wa yatima.


Ee BWANA, unihukumu mimi, Maana nimekwenda kwa ukamilifu wangu, Nami nimemtumaini BWANA bila wasiwasi.


Ee BWANA, uwapinge hao wanaonipinga, Upigane nao wanaopigana nami.


Uamke, uwe macho ili kunipatia hukumu Kwa ajili ya madai yangu, Mungu wangu na Bwana wangu.


Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.


Kwa maana umenifanyia hukumu na haki Umeketi kitini pa enzi ukihukumu kwa haki.


Ole wangu, mama yangu, kwa kuwa umenizaa mtu wa kuteta, na mtu wa kushindana na dunia yote! Mimi sikukopesha kwa riba, wala watu hawakunikopesha kwa riba; lakini kila mmoja wao hunilaani.


Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa.


Umekiona kisasi chao chote, Na mashauri yao yote juu yangu.


Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.