Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 3:24 - Swahili Revised Union Version

BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yangu hivyo nitamwekea tumaini langu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yangu hivyo nitamwekea tumaini langu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu ndiye hazina yangu hivyo nitamwekea tumaini langu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nimeiambia nafsi yangu, “Mwenyezi Mungu ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nimeiambia nafsi yangu, “bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 3:24
25 Marejeleo ya Msalaba  

Wakapata msaada juu yao, nao Wahajiri walitiwa mikononi mwao, na wote waliokuwa pamoja nao; kwa kuwa walimlingana Mungu pale vitani; naye akayatakabali maombi yao, kwa sababu walimtumaini yeye.


Tazama, ataniua; sina tumaini; Ila hata hivyo nitaithibitisha njia yangu mbele yake.


Naye Mwenyezi atakuwa hazina yako, Atakuwa ni fedha ya thamani kwako.


BWANA ndiye aliye fungu langu, Ninaahidi kuyatii maneno yake.


Ee Israeli, umtarajie BWANA; Maana kwa BWANA kuna fadhili, Na kwake kuna ukombozi mwingi.


BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.


BWANA ndiye fungu la posho langu, Na la kikombe changu; Wewe unayaamua maisha yangu.


Iweni hodari, na mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja BWANA.


Tazama, jicho la BWANA li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili zake.


Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.


Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumainie Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.


Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Maana nitamsifu tena, Aliye msaada wangu, Na Mungu wangu.


Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu.


Lakini mimi nitakutumainia daima, Nitaendelea kukusifu zaidi na zaidi.


Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele.


Ee BWANA wa majeshi, Heri mwanadamu anayekutumaini Wewe.


Katika wingi wa mawazo ya moyoni mwangu, Faraja zako zinaifurahisha roho yangu.


Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila la urithi wake; BWANA wa majeshi ndilo jina lake.


Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila la urithi wake; BWANA wa majeshi ndilo jina lake.


Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini.


Lakini mimi, nitamtazamia BWANA; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia.


Na tena Isaya anena, Litakuwako shina la Yese, Naye aondokeaye kuwatawala Mataifa; Ndiye Mataifa watakayemtumaini.


Wala wasiwe na urithi kati ya ndugu zao; BWANA ndiye urithi wao, kama alivyowaambia.


na kupitia kwake mmekuwa wenye kumwamini Mungu, aliyemfufua katika wafu akampa utukufu; hata imani yenu na tumaini lenu liwe kwa Mungu.


Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika BWANA, Mungu wake.