Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Maombolezo 2:18 - Swahili Revised Union Version

Mioyo yao ilimlilia Bwana; Ee ukuta wa binti Sayuni! Machozi na yachuruzike kama mto Mchana na usiku; Usijipatie kupumzika; Mboni ya jicho lako isikome.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu! Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku! Lia na kuomboleza bila kupumzika!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu! Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku! Lia na kuomboleza bila kupumzika!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kuta zako, ee mji wa Siyoni, zimlilie Mwenyezi-Mungu! Machozi na yatiririke kama mto mchana na usiku! Lia na kuomboleza bila kupumzika!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mioyo ya watu inamlilia Bwana. Ee ukuta wa Binti Sayuni, machozi yako na yatiririke kama mto usiku na mchana; usijipe nafuu, macho yako yasipumzike.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mioyo ya watu inamlilia Bwana. Ee ukuta wa Binti Sayuni, machozi yako na yatiririke kama mto usiku na mchana; usijipe nafuu, macho yako yasipumzike.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mioyo yao ilimlilia Bwana; Ee ukuta wa binti Sayuni! Machozi na yachuruzike kama mto Mchana na usiku; Usijipatie kupumzika; Mboni ya jicho lako isikome.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Maombolezo 2:18
14 Marejeleo ya Msalaba  

Macho yangu yachuruzika mito ya machozi, Kwa sababu hawaitii sheria yako.


Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee BWANA, uitike; Nitazishika amri zako.


Bali kama hamtaki kusikia, roho yangu italia kwa siri, kwa sababu ya kiburi chenu; na jicho langu litalia sana na kutoka machozi mengi, kwa kuwa kundi la BWANA limechukuliwa mateka.


Nawe utawaambia neno hili, Macho yangu na yatiririke machozi, usiku na mchana, wala yasikome; kwa maana bikira, binti ya watu wangu, amevunjika mavunjiko makuu, kwa jeraha lisiloponyeka.


Kwa maana nimesikia sauti, kama sauti ya mwanamke wakati wa uchungu wake, na sauti yake aumwaye, kama mwanamke azaaye mtoto wake wa kwanza, sauti ya binti Sayuni, atwetaye kupata pumzi, na kunyosha mikono yake, akisema, Ole wangu, sasa! Kwa maana roho yangu inazimia mbele ya wauaji.


Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu kuwa chemchemi ya machozi, ili nipate kulia mchana na usiku kwa ajili yao waliouawa wa binti ya watu wangu!


Mimi ninayalilia mambo hayo; Jicho langu, jicho langu linachuruzika machozi; Kwa kuwa mfariji yuko mbali nami, Ambaye ilimpasa kunihuisha nafsi; Watoto wangu wameachwa peke yao, Kwa sababu huyo adui ameshinda.


Hulia sana wakati wa usiku, Na machozi yake yapo mashavuni; Miongoni mwa wote waliompenda Hakuna hata mmoja amfarijiye; Rafiki zake wote wamemtenda hila, Wamekuwa adui zake.


BWANA amekusudia kuuharibu Ukuta wa binti Sayuni; Ameinyosha hiyo kamba, Hakuuzuia mkono wake usiangamize; Bali amefanya boma na ukuta kuomboleza; Zote pamoja hudhoofika.


Wala hawakunililia kwa moyo, lakini wanalalamika vitandani mwao; hujikutanisha ili kupata nafaka na divai; huniasi mimi.


Kwa maana jiwe litapiga kelele katika ukuta, nayo boriti katika miti italijibu.