Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 29:2 - Swahili Revised Union Version

ndipo nitamwudhi Arieli; kutakuwapo maombolezo na kilio; naye atakuwa kwangu kama Arieli.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

lakini mimi Mungu nitauhuzunisha Yerusalemu, nako kutakuwa na vilio na maombolezo, mji wenyewe utakuwa kama madhabahu iliyolowa damu ya watu waliouawa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

lakini mimi Mungu nitauhuzunisha Yerusalemu, nako kutakuwa na vilio na maombolezo, mji wenyewe utakuwa kama madhabahu iliyolowa damu ya watu waliouawa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

lakini mimi Mungu nitauhuzunisha Yerusalemu, nako kutakuwa na vilio na maombolezo, mji wenyewe utakuwa kama madhabahu iliyolowa damu ya watu waliouawa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hata hivyo nitauzingira Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hata hivyo nitauzunguka Arieli kwa jeshi, utalia na kuomboleza, utakuwa kwangu kama mahali pa kuwashia moto madhabahuni.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

ndipo nitamwudhi Arieli; kutakuwapo maombolezo na kilio; naye atakuwa kwangu kama Arieli.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 29:2
19 Marejeleo ya Msalaba  

Sikukuu zenu za mwezi mpya na karamu zenu zilizoamriwa, nafsi yangu yazichukia; mambo hayo yanilemea; nimechoka kuyachukua.


siku hii ya leo atasimama huko Nobu; anatikisa mkono wake juu ya mlima wa binti Sayuni, mlima wa Yerusalemu.


Wakati wa jioni, tazama, kuna hofu; Na kabla ya mapambazuko hawako; Hilo ndilo fungu lao watutekao, Na ajali yao wanaotunyang'anya mali zetu.


Na malango yake yatalia na kuomboleza, naye atakuwa ukiwa, atakaa chini.


Upanga wa BWANA umeshiba damu, umejazwa mafuta, kwa damu ya wana-kondoo na mbuzi, kwa mafuta ya figo za kondoo dume; maana BWANA ana dhabihu huko Bozra, machinjo makubwa katika nchi ya Edomu.


Ndipo Eliakimu, mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba ya mfalme, na Shebna, mwandishi, na Yoa, mwana wa Asafu mwenye kuandika kumbukumbu, wakaenda kwa Hezekia, na nguo zao zikiwa zimeraruliwa, wakamwambia Hezekia maneno ya yule kamanda.


Wakamwambia, Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, na aibu, na matukano; maana watoto wako tayari kuzaliwa, wala hapana nguvu za kuwazaa.


Bwana amekuwa mfano wa adui, Amemmeza Israeli; Ameyameza majumba yake yote, Ameziharibu ngome zake; Tena amemzidishia binti Yuda Matanga na maombolezo.


Kwa sababu hiyo nimemwaga ghadhabu yangu juu yao; nimewateketeza kwa moto wa hasira yangu; nami nimeileta njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao, asema Bwana MUNGU.


Na wewe, mwanadamu, Bwana MUNGU asema hivi; Sema na ndege wa kila namna, na kila mnyama wa porini, Jikusanyeni, mje; jikusanyeni pande zote mwijie karamu yangu ya kafara ninayoandaa kwa ajili yenu, naam, karamu kuu ya kafara juu ya milima ya Israeli, mpate kula nyama na kunywa damu.