Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Isaya 3:26 - Swahili Revised Union Version

26 Na malango yake yatalia na kuomboleza, naye atakuwa ukiwa, atakaa chini.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

26 Malango ya mji yatalia na kuomboleza; nao mji utakuwa kama mwanamke aliyepokonywa kila kitu, ameketi mavumbini.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

26 Malango ya mji yatalia na kuomboleza; nao mji utakuwa kama mwanamke aliyepokonywa kila kitu, ameketi mavumbini.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

26 Malango ya mji yatalia na kuomboleza; nao mji utakuwa kama mwanamke aliyepokonywa kila kitu, ameketi mavumbini.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia, ataketi mavumbini akiwa fukara.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

26 Malango ya Sayuni yataomboleza na kulia, ataketi mavumbini akiwa fukara.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

26 Na malango yake yatalia na kuomboleza, naye atakuwa ukiwa, atakaa chini.

Tazama sura Nakili




Isaya 3:26
19 Marejeleo ya Msalaba  

Kisha wakaketi ardhini pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lolote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.


Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni.


Piga yowe, Ee lango; lia, Ee mji; Ee Ufilisti enyi wote, umeyeyuka kabisa; Maana moshi unakuja toka kaskazini, Wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.


ndipo nitamwudhi Arieli; kutakuwapo maombolezo na kilio; naye atakuwa kwangu kama Arieli.


maana jumba la mfalme litaachwa; mji uliokuwa na watu wengi utakuwa hauna mtu; kilima na mnara utakuwa makao ya wanyama milele, furaha ya punda mwitu, malisho ya makundi ya kondoo;


Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani.


Haya, shuka, keti mavumbini, Ewe bikira, binti Babeli; Keti chini pasipo kiti cha enzi, Ewe binti wa Wakaldayo; Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.


Ndipo nilipouliza, Ee Bwana, hata lini? Naye akanijibu, Hadi miji itakapokuwa ukiwa, haina wenyeji, na nyumba zitakapokuwa hazina watu, na nchi hii itakapokuwa ganjo kabisa;


Yuda huomboleza, Na malango yake yamelegea; Wameketi chini wamevaa kaniki; Na kilio cha Yerusalemu kimepaa juu.


Wajane wao wameongezeka kwangu kuliko mchanga wa bahari; nimeleta mwenye kuteka wakati wa adhuhuri juu ya mama wa vijana; nimeleta uchungu na hofu kuu impate ghafla.


Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa, Huo uliokuwa umejaa watu! Jinsi alivyokuwa kama mjane, Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa! Binti mfalme kati ya majimbo, Jinsi alivyoshikwa shokoa!


Njia za Sayuni zaomboleza, Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu; Malango yake yote yamekuwa ukiwa, Makuhani wake hupiga kite; Wanawali wake wanahuzunika; Na yeye mwenyewe huona uchungu.


Wazee wa binti Sayuni huketi chini, Hunyamaza kimya; Wametupa mavumbi juu ya vichwa vyao, Wamejivika viunoni nguo za magunia; Wanawali wa Yerusalemu huinama vichwa vyao Kuielekea nchi.


BWANA amekusudia kuuharibu Ukuta wa binti Sayuni; Ameinyosha hiyo kamba, Hakuuzuia mkono wake usiangamize; Bali amefanya boma na ukuta kuomboleza; Zote pamoja hudhoofika.


Na miji yote yenye watu itakuwa maganjo, nayo nchi itakuwa ukiwa; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA.


Ndipo wakuu wote wa bahari watashuka kutoka viti vyao vya enzi, na kuweka upande mavazi yao, na kuvua nguo zao zilizotiwa taraza; watajivika wakitetemeka; wataketi na kutetemeka kila dakika, na kukustaajabia,


Kwa maana majeraha yake hayaponyeki; Maana msiba umeijia hata Yuda, Unalifikia lango la watu wangu, Naam, hata Yerusalemu.


Tuliwapigia filimbi, wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.


watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiwa kwako.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo