Hosea 8:2 - Swahili Revised Union Version Watanililia, Mungu wangu, sisi Israeli tunakujua. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Waisraeli hunililia wakisema: ‘Mungu wetu, sisi tunakujua.’ Biblia Habari Njema - BHND Waisraeli hunililia wakisema: ‘Mungu wetu, sisi tunakujua.’ Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Waisraeli hunililia wakisema: ‘Mungu wetu, sisi tunakujua.’ Neno: Bibilia Takatifu Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’ Neno: Maandiko Matakatifu Israeli ananililia, ‘Ee Mungu wetu, tunakukubali!’ BIBLIA KISWAHILI Watanililia, Mungu wangu, sisi Israeli tunakujua. |
Walakini katika makosa yake Yeroboamu mwana wa Nebati, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli, Yehu hakutoka katika kuyafuata, yaani, ndama za dhahabu zilizokuwako katika Betheli na Dani.
Msitumainie maneno ya uongo, mkisema, Hekalu la BWANA, Hekalu la BWANA, Hekalu la BWANA ndiyo haya.
Nitakwenda zangu niparudie mahali pangu, hata watakapoungama makosa yao na kunitafuta uso wangu; katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.
Wakuu wake huhukumu ili wapate rushwa, na makuhani wake hufundisha ili wapate ijara, na manabii wake hubashiri ili wapate fedha; ila hata hivyo watamtegemea BWANA, na kusema, Je! Hayupo BWANA katikati yetu? Hapana neno baya lolote litakalotufikia.
Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
Wanakiri ya kwamba wanamjua Mungu, bali kwa matendo yao wanamkana; ni wenye machukizo, waasi, wala hawafai kwa tendo lolote jema.
Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake.