Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




2 Wafalme 10:16 - Swahili Revised Union Version

16 Akasema, Fuatana nami, ukaone wivu wangu kwa BWANA. Wakampandisha garini mwake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

16 Akamwambia, “Fuatana nami ili ujionee jinsi nilivyo mwaminifu kwa Mwenyezi-Mungu.” Basi, wakasafiri pamoja garini mwake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

16 Akamwambia, “Fuatana nami ili ujionee jinsi nilivyo mwaminifu kwa Mwenyezi-Mungu.” Basi, wakasafiri pamoja garini mwake.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

16 Akamwambia, “Fuatana nami ili ujionee jinsi nilivyo mwaminifu kwa Mwenyezi-Mungu.” Basi, wakasafiri pamoja garini mwake.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

16 Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake la vita.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

16 Yehu akasema, “Twende pamoja ukaone wivu wangu kwa ajili ya bwana.” Hivyo wakasafiri pamoja kwenye gari lake.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

16 Akasema, Fuatana nami, ukaone wivu wangu kwa BWANA. Wakampandisha garini mwake.

Tazama sura Nakili




2 Wafalme 10:16
13 Marejeleo ya Msalaba  

Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya BWANA Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe.


Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya BWANA, Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu waiondoe.


Na itakuwa atakayeokoka na upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua; na atakayeokoka na upanga wa Yehu, Elisha atamwua.


Naye alipofika Samaria, aliwaua wote wa Ahabu waliokuwa wamebakia katika Samaria, hata akamwangamiza, sawasawa na neno la BWANA alilomwambia Eliya.


Lakini Yehu hakuangalia, aende katika sheria ya BWANA, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote; hakutoka katika makosa ya Yeroboamu, ambayo kwa hayo aliwakosesha Israeli.


Mwingine na akusifu wala si kinywa chako mwenyewe; Mtu mgeni wala si midomo yako wewe.


Nao huja kwako kama watu wajavyo, nao hukaa mbele yako kama watu wangu, nao husikia maneno yako, wasiyatende; maana kwa vinywa vyao hujifanya kuwa wenye upendo mwingi, lakini mioyo yao inatafuta faida yao.


Mungu akakutana na Balaamu; naye Balaamu akamwambia, Nimetengeneza madhabahu saba, nami nimetoa sadaka ng'ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.


Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu.


Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.


Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo