(kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema, Wana wa Yuda na wafundishwe haya,
Hesabu 21:14 - Swahili Revised Union Version Kwa hiyo imesemwa katika Kitabu cha Vita vya BWANA, Wahebu katika Sufa, Na bonde za Arnoni, Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Kwa sababu hiyo, imeandikwa katika kitabu cha vita vya Mwenyezi-Mungu: “Mji wa Wahebu nchini Sufa, na mabonde ya Arnoni, Biblia Habari Njema - BHND Kwa sababu hiyo, imeandikwa katika kitabu cha vita vya Mwenyezi-Mungu: “Mji wa Wahebu nchini Sufa, na mabonde ya Arnoni, Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Kwa sababu hiyo, imeandikwa katika kitabu cha vita vya Mwenyezi-Mungu: “Mji wa Wahebu nchini Sufa, na mabonde ya Arnoni, Neno: Bibilia Takatifu Ndiyo sababu Kitabu cha Vita vya Mwenyezi Mungu kinasema: “Wahebu nchini Sufa, na mabonde, Mto Arnoni, Neno: Maandiko Matakatifu Ndiyo sababu Kitabu cha Vita vya bwana kinasema: “…Mji wa Wahebu nchini Seifa na mabonde ya Arnoni, BIBLIA KISWAHILI Kwa hiyo imesemwa katika Kitabu cha Vita vya BWANA, Wahebu katika Sufa, Na bonde za Arnoni, |
(kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Yashari), akasema, Wana wa Yuda na wafundishwe haya,
Na binti za Moabu watakuwa kama ndege warukao huku na huko, kama kiota cha ndege waliotiwa hofu, kwenye vivuko vya Arnoni.
Kutoka huko wakasafiri, wakapanga upande wa pili wa Arnoni, ulio jangwani, utokao katika mpaka wa Waamori; maana, Arnoni ndio mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
Na materemko ya hizo bonde Kwenye kuteremkia maskani ya Ari, Na kutegemea mpaka wa Moabu.
Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.
Ondokeni, mshike safari yenu, mvuke bonde la Arnoni; tazama, nimemtia Sihoni Mwamori mfalme wa Heshboni mkononi mwako, na nchi yake; anzeni kuimiliki, mshindane naye katika mapigano.
Ndipo jua likasimama, na mwezi ukatulia, Hadi hilo taifa lilipokuwa limekwisha jilipiza kisasi juu ya adui zao. Hayo, je! Hayakuandikwa ndani ya kitabu cha Yashari? Basi jua likasimama kimya katikati ya mbingu, wala halikufanya haraka kuchwa kama muda wa siku nzima.
Kisha Sauli akamwambia Daudi, Tazama, binti yangu mkubwa, Merabu, huyu nitakupa wewe ili umwoe; ila na wewe uniwie hodari wa vita, na kuvipiga vita vya BWANA. Maana Sauli alisema moyoni mwake, Mkono wangu usiwe juu yake, bali mkono wa Wafilisti na uwe juu yake.