Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hesabu 16:4 - Swahili Revised Union Version

Musa aliposikia maneno haya, akaanguka kifudifudi;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mose aliposikia hayo, alijitupa chini kifudifudi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mose aliposikia hayo, alijitupa chini kifudifudi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mose aliposikia hayo, alijitupa chini kifudifudi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Musa aliposikia jambo hili, akaanguka kifudifudi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Musa aliposikia jambo hili, akaanguka kifudifudi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Musa aliposikia maneno haya, akaanguka kifudifudi;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hesabu 16:4
7 Marejeleo ya Msalaba  

Tena ikawa, walipokuwa wakiwaua, nami nikaachwa, nilianguka kifudifudi, nikalia, nikasema, Ee Bwana MUNGU! Utaangamiza mabaki yote ya Israeli, wakati wa kumwaga ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?


Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya kusanyiko la wana wa Israeli.


Nao wakaanguka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?


Ondokeni kati ya mkutano, ili niwaangamize mara moja. Wao wakaanguka kifudifudi.


kisha akanena na Kora na mkutano wake wote, akawaambia, Asubuhi BWANA ataonesha ni kina nani walio wake, kisha ni nani aliye mtakatifu, tena ni nani atakayemkaribisha kwake; maana, yeye atakayemchagua ndiye atakayemsongeza kwake.


Musa na Haruni wakatoka pale palipokuwa mkutano, wakaenda hadi mlangoni pa hema ya kukutania, wakaanguka kifudifudi; utukufu wa BWANA ukawatokea.


Yoshua akararua mavazi yake, akaanguka kifudifudi mbele ya sanduku la BWANA hadi jioni, yeye na wazee wa Israeli; wakatia mavumbi vichwani mwao.