Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 6:6 - Swahili Revised Union Version

Basi wale mawaziri na viongozi wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia hivi, Mfalme Dario, uishi milele.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, hao wakuu na maliwali kwa pamoja, wakamwendea mfalme na kumwambia, “Uishi ee mfalme Dario!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, hao wakuu na maliwali kwa pamoja, wakamwendea mfalme na kumwambia, “Uishi ee mfalme Dario!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, hao wakuu na maliwali kwa pamoja, wakamwendea mfalme na kumwambia, “Uishi ee mfalme Dario!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi, wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi wasimamizi na wakuu wakaingia kwa mfalme kama kikundi wakasema, “Ee Mfalme Dario, uishi milele!

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Kisha wale wakuu na watawala nchi wakamwendea mfalme na kumpigia shangwe, wakamwambia: Mfalme Dario na uwe mwenye uzima kale na kale!

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 6:6
13 Marejeleo ya Msalaba  

Nikamwambia mfalme, Mfalme na aishi milele; kwani uso wangu usiwe na huzuni, iwapo mji, ulio mahali pa makaburi ya baba zangu, unakaa ukiwa, na malango yake yameteketezwa kwa moto?


Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu, Kwa kuwa waliniotea ili waniue.


Hadi lini mtamshambulia mtu, Mpate kumwua ninyi nyote pamoja? Kama ukuta unaoinama, Kama ua ulio tayari kuanguka,


Ndipo hao Wakaldayo wakamwambia mfalme, kwa lugha ya Kiaramu, Ee Mfalme, uishi milele; tuambie sisi watumishi wako ile ndoto, nasi tutakuonesha tafsiri yake.


Wakajibu, wakamwambia mfalme Nebukadneza, Ee mfalme, uishi milele.


Basi malkia, kwa sababu ya maneno ya mfalme na ya wakuu wake, akaingia katika nyumba ya karamu; malkia akanena, akasema, Ee mfalme, uishi milele; fikira zako zisikufadhaishe; wala uso wako usibadilike.


Basi watu hao wakakusanyika pamoja, wakamwona Danieli akiomba dua, mbele za Mungu wake na kusihi.


Ndipo Danieli akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele.


Naye alipoitwa, Tertulo akaanza kumshitaki, akisema, Kwa kuwa mnapata amani nyingi chini yako, Feliki mtukufu, na kwa uongozi wako mambo mabaya yanasuluhishwa kwa ajili ya taifa hili,