Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Danieli 2:20 - Swahili Revised Union Version

Danieli akajibu, akasema, Na lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; kwa kuwa hekima na uweza ni wake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

akasema, “Na litukuzwe milele na milele jina lake Mungu. Hekima na nguvu ni vyake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

akasema, “Na litukuzwe milele na milele jina lake Mungu. Hekima na nguvu ni vyake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

akasema, “Na litukuzwe milele na milele jina lake Mungu. Hekima na nguvu ni vyake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

na akasema: “Lihimidiwe jina la Mungu milele na milele; hekima na uweza ni vyake.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Hivi ndivyo, Danieli alivyosema: Jina lake Mungu litukuzwe kale na kale! Kwani yeye ni mwenye ujuzi na uwezo!

Tazama sura
Tafsiri zingine



Danieli 2:20
25 Marejeleo ya Msalaba  

Ahimidiwe Mungu Aliye Juu Sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.


Na ahimidiwe BWANA, aliyewapa watu wake Israeli kustarehe, vile vile kama yote aliyoyaahidi. Halikukosa kupatikana neno lolote katika ahadi yake njema, aliyoahidi kwa mkono wa Musa, mtumishi wake.


Ndipo Daudi akawaambia kusanyiko lote, Haya, mhimidini BWANA, Mungu wenu. Basi kusanyiko lote wakamhimidi BWANA, Mungu wa baba zao, wakainamisha vichwa vyao, wakamsujudia BWANA, na mfalme naye.


Naye alipokwisha kufanya shauri na watu, akawaweka wale watakaomwimbia BWANA, na kumsifu katika uzuri wa utakatifu, wakitoka mbele ya jeshi, na kusema, Mshukuruni BWANA; kwa maana fadhili zake ni za milele.


Ndipo Walawi, Yeshua na Kadmieli, na Bani, na Hashabneya, na Sherebia, na Hodia, na Shebania, na Pethahia, wakasema, Simameni, mkamhimidi BWANA, Mungu wenu, tangu milele na hata milele. Na lihimidiwe jina lako tukufu, lililotukuka kuliko baraka zote na sifa zote.


Hekima na amri zina yeye [Mungu]; Yeye anayo ushauri na fahamu.


Haleluya. Enyi watumishi wa BWANA, sifuni, Lisifuni jina la BWANA.


Jina la BWANA lihimidiwe Tangu leo na hata milele.


Bali sisi tutamhimidi BWANA, Tangu leo na hata milele.


Bwana wetu ni mkuu na mwingi wa nguvu, Akili zake hazina mpaka.


Na atukuzwe BWANA, Mungu wa Israeli, Tangu milele hata milele. Amina na Amina.


Atoaye dhabihu za kushukuru, Ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, Nitamwonesha wokovu wa Mungu.


Mara moja amenena Mungu; Mara mbili nimeyasikia haya, Ya kuwa nguvu zina Mungu,


Ushauri ni wangu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu.


mkuu wa mashauri, muweza katika kutenda; ambaye macho yake yamefumbuka juu ya njia zote za wanadamu, kumpa kila mtu kwa kadiri ya njia zake, na kwa kadiri ya matunda ya matendo yake,


Tazama, una hekima kuliko Danieli; hapana neno la siri watu wawezalo kukuficha;


Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]


Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu;


wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.