Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




2 Samueli 22:36 - Swahili Revised Union Version

Nawe umenipa ngao ya wokovu wako; Na unyenyekevu wako umenikuza.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Umenipa ngao yako ya kuniokoa; msaada wako umenifanya mkuu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Umenipa ngao yako ya kuniokoa; msaada wako umenifanya mkuu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Umenipa ngao yako ya kuniokoa; msaada wako umenifanya mkuu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hufanya msaada wa wokovu wako kuwa ngao yangu; msaada wako umeniinua niwe mkuu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nawe umenipa ngao ya wokovu wako; Na unyenyekevu wako umenikuza.

Tazama sura
Tafsiri zingine



2 Samueli 22:36
8 Marejeleo ya Msalaba  

nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;


Baada ya mambo hayo neno la BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako itakuwa kubwa sana.


katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki lango la adui zao;


BWANA na awaongeze ninyi, Ninyi na watoto wenu.


Nawe umenipa ngao ya wokovu wako, Mkono wako wa kulia umenitegemeza, Na unyenyekevu wako umenikuza.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.


Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;