Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wafalme 4:1 - Swahili Revised Union Version

Basi mfalme Sulemani akawa mfalme juu ya Israeli wote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Solomoni alikuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli,

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Solomoni alikuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli,

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Solomoni alikuwa mfalme wa nchi yote ya Israeli,

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi Mfalme Sulemani akatawala Israeli yote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi Mfalme Sulemani akatawala Israeli yote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Basi mfalme Sulemani akawa mfalme juu ya Israeli wote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wafalme 4:1
14 Marejeleo ya Msalaba  

Basi Yoabu alikuwa akiongoza jeshi lote la Israeli; na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa akiwaongoza Wakerethi, na Wapelethi;


Huko Hebroni alitawala miaka saba na miezi sita; na katika Yerusalemu alitawala miaka thelathini na tatu juu ya Israeli wote na Yuda.


Daudi akatawala juu ya Israeli wote; naye Daudi akawafanyia hukumu na haki watu wake wote.


Lakini sitauondoa ufalme wote pia; nitampa mwana wako kabila moja, kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu, na kwa ajili ya Yerusalemu niliouchagua.


Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee waliokuwa wakisimama mbele ya Sulemani, baba yake, alipokuwa hai, akasema, Mwanipa shauri gani ili niwajibu watu hawa?


Na Israeli wote wakapata habari za hukumu ile aliyoihukumu mfalme wakamwogopa mfalme; maana waliona ya kuwa hekima ya Mungu ilikuwa ndani yake, ili afanye hukumu.


Na hawa ndio wakuu aliokuwa nao; Azaria mwana wa Sadoki, kuhani,


Hao wote, watu wa vita, askari stadi, wakaja Hebroni wakiwa na nia moja ya kumtawaza Daudi awe mfalme juu ya Israeli wote; tena wote waliosalia wa Israeli nao walikuwa na moyo mmoja kwamba wamtawaze Daudi.


Basi Sulemani akatoka mahali pa juu pa Gibeoni, toka mbele ya Hema la kukutania, akaja mpaka Yerusalemu; akatawala Israeli.


Sulemani akatawala katika Yerusalemu juu ya Israeli wote miaka arubaini.


Je! Sulemani, mwana wa Daudi, hakufanya dhambi kwa kutenda hayo? Lakini katika mataifa mengi hapakuwa na mfalme mwingine mfano wake. Tena alipendwa na Mungu wake, naye Mungu akamfanya mfalme juu ya Israeli; lakini wanawake wageni walimkosesha hata yeye.


Mimi, Mhubiri, nilikuwa Mfalme wa Israeli katika Yerusalemu.