Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 9:9 - Swahili Revised Union Version

9 BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa, Naam, ngome kwa nyakati za shida.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

9 Mwenyezi-Mungu ni ngome ya watu wanaoonewa; yeye ni ngome nyakati za taabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

9 Mwenyezi-Mungu ni ngome ya watu wanaoonewa; yeye ni ngome nyakati za taabu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

9 Mwenyezi-Mungu ni ngome ya watu wanaoonewa; yeye ni ngome nyakati za taabu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

9 Mwenyezi Mungu ni kimbilio la wanaodhulumiwa, ni ngome imara wakati wa shida.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

9 bwana ni kimbilio la watu wanaoonewa, ni ngome imara wakati wa shida.

Tazama sura Nakili




Zaburi 9:9
26 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo miti yote ya mwituni iimbe kwa furaha, Mbele za BWANA, Kwa maana anakuja kuihukumu nchi.


Utuletee msaada juu ya mtesi, Maana wokovu wa binadamu haufai.


Utazame mkono wangu wa kulia ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.


BWANA ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.


BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.


Kimbilio langu utanilinda nisipate mateso, Utanizungusha nyimbo za kufurahia wokovu wangu.


Na wokovu wa wenye haki una BWANA; Yeye ni ngome yao wakati wa taabu.


Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.


BWANA wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.


Mungu katika majumba yake Amejijulisha kuwa ngome.


Uniite siku ya mateso; Nitakuokoa, nawe utanitukuza.


Enyi watu, mtumainini sikuzote, Ifunueni mioyo yenu mbele zake; Mungu ndiye kimbilio letu.


Watu na wakushukuru, Ee Mungu, Watu wote na wakushukuru.


Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na fikira Ndiye Mungu aliye mwenye haki.


Semeni katika mataifa, BWANA ametamalaki; Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike, Atawahukumu watu kwa adili.


Mbele za BWANA; Kwa maana anakuja kuihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa uaminifu, Na mataifa kwa adili.


Jina la BWANA ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.


Na mwanadamu atakuwa kama mahali pa kujificha na upepo, na mahali pa kujisitiri na dhoruba; kama mito ya maji mahali pakavu, kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi yenye uchovu.


Naye atakuwa ni mahali patakatifu; bali ni jiwe la kujikwaza na mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili, na mtego na tanzi kwa wenyeji wa Yerusalemu.


BWANA ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.


Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga kwa mawe waliotumwa kwako, mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako kama vile kuku awakusanyavyo vifaranga wake chini ya mbawa zake, wala hamkutaka.


Mungu wa milele ndiye makazi yako, Na mikono ya milele i chini yako. Na mbele yako amemsukumia mbali adui; Akasema, Angamiza.


ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;


Tufuate:

Matangazo


Matangazo