Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 6:10 - Swahili Revised Union Version

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, Watarudi nyuma, kwa ghafla wataaibika.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

10 Maadui zangu wote wataaibika na kufadhaika; watarudi nyuma na kuaibishwa ghafla.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

10 Maadui zangu wote wataaibika na kufadhaika; watarudi nyuma na kuaibishwa ghafla.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

10 Maadui zangu wote wataaibika na kufadhaika; watarudi nyuma na kuaibishwa ghafla.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma na waaibishwe kwa ghafula.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.

Tazama sura Nakili




Zaburi 6:10
23 Marejeleo ya Msalaba  

Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, BWANA, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa BWANA.


Rudini, nawasihi, lisiwe neno la udhalimu; Naam, rudini tena, neno langu ni la haki.


Asiye haki ataona na kusikitika, Atasaga meno yake na kuondoka, Matumaini ya wasio haki hupotea.


Adui zake nitawavika aibu, Bali juu yake taji lake litasitawi.


Ndipo atakaposema nao kwa hasira yake, Na kuwafadhaisha kwa ghadhabu yake, akisema:


Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; Wataaibika watendao uhaini bila sababu.


Waaibishwe, wafedheheshwe pamoja, Wanaoifurahia hali yangu mbaya. Wavikwe aibu na fedheha, Wanaojikuza juu yangu.


Wewe, Mungu, uwapatilize, Na waanguke kwa mashauri yao. Uwatoe nje kwa ajili ya wingi wa makosa yao, Kwa maana wamekuasi Wewe.


Mwenzangu amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, Amelivunja agano lake.


BWANA uondoke kwa hasira yako; Ujiinue Juu ya ujeuri wa watesi wangu; Uamke kwa ajili yangu; Umeamuru hukumu.


Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu. Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.


Ulimi wangu nao utasimulia Haki yako mchana kutwa. Kwa maana wameaibishwa, Wametahayarika, wanaonitakia mabaya.


Namna gani wameangamizwa punde! Wakafutiliwa mbali kwa vitisho.


Unifanyie ishara ya wema, Wanichukiao waione na kuaibishwa. Kwa kuwa Wewe, BWANA, Umenisaidia na kunifariji.


Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafla, wala hapati dawa.


BWANA, mkono wako umeinuliwa, lakini hawaoni; lakini watauona wivu wako kwa ajili ya watu wako, nao watatahayari; naam, moto utawala adui zako.


Lakini BWANA yuko pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawatafaulu wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe.


Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.


Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla, kama vile uchungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo