Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 5:5 - Swahili Revised Union Version

5 Wajivunao hawatasimama mbele za macho yako; Unawachukia wote watendao uovu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Wenye majivuno hawastahimili mbele yako; wewe wawachukia wote watendao maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Wenye majivuno hawastahimili mbele yako; wewe wawachukia wote watendao maovu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Wenye majivuno hawastahimili mbele yako; wewe wawachukia wote watendao maovu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, unawachukia wote watendao mabaya.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, unawachukia wote watendao mabaya.

Tazama sura Nakili




Zaburi 5:5
21 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.


Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.


BWANA humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.


BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama?


Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu; Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo, Hakuna atendaye mema.


Maana niliwaonea wivu wenye kujivuna, Nilipoiona hali ya amani ya wasio haki.


Niliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe.


Mtu mjinga hayatambui hayo, Wala mpumbavu hayafahamu.


Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini; Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?


Enyi wajinga, hata lini mtapenda ujinga? Na wenye dharau kupenda dharau yao, Na wapumbavu kuchukia maarifa?


Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.


Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; Bali humpenda mtu afuatiaye wema.


Enyi wajinga, fahamuni werevu, Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.


Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.


Uovu wao wote u katika Gilgali; maana huko niliwachukia; kwa sababu ya uovu wa matendo yao nitawafukuza watoke katika nyumba yangu; sitawapenda tena; wakuu wao wote ni waasi.


Nanyi msiende kwa kuzifuata desturi za taifa, niitoayo mbele yenu; kwa kuwa wao waliyafanya mambo hayo yote, na kwa ajili ya hayo niliwachukia.


Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye;


Nami nikawakatilia mbali wachungaji watatu katika mwezi mmoja; maana nafsi yangu ilikuwa imechoka kwa ajili yao, na nafsi zao pia walinichukia.


Kisha atawaambia na wale walioko katika mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;


Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo