Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 23:1 - Swahili Revised Union Version

1 BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

1 Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

1 Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

1 Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

1 Mwenyezi Mungu ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

1 bwana ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

1 BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

Tazama sura Nakili




Zaburi 23:1
25 Marejeleo ya Msalaba  

Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha BWANA.


Kisha akawaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani.


Na sisi tulio watu wako, Na kondoo za malisho yako, Tutakushukuru milele; Tutazisimulia sifa zako kizazi hadi kizazi.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Atalilisha kundi lake kama mchungaji, Atawakusanya wana-kondoo mikononi mwake; Na kuwachukua kifuani mwake, Nao wanyonyeshao atawaongoza polepole.


Lisikieni neno la BWANA, enyi mataifa, litangazeni visiwani mbali; mkaseme, Aliyemtawanya Israeli atamkusanya, na kumlinda, kama mchungaji alindavyo kundi lake.


Nami nitawalisha malisho mema, pa juu ya milima ya mahali palipoinuka pa Israeli litakuwa zizi lao; huko watalala katika zizi jema; nao watakula malisho mema, juu ya milima ya Israeli.


Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye asili yake imekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.


Naye atasimama, na kulisha kundi lake kwa nguvu za BWANA, kwa enzi ya jina la BWANA, Mungu wake; nao watakaa; maana sasa atakuwa mkuu hadi miisho ya dunia.


Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.


Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.


Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;


Yeye ambaye hakumhurumia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje pia kutupa chochote kingine pamoja naye?


Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.


Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu Mchungaji Mkuu wa kondoo, kwa damu ya agano la milele, yeye Bwana wetu Yesu,


Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.


Na Mchungaji mkuu atakapodhihirishwa, mtalipokea taji la utukufu, lile lisilokauka.


Kwa maana huyo Mwana-kondoo, aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga, naye atawaongoza kwenye chemchemi za maji yenye uhai, na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo