Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 139:3 - Swahili Revised Union Version

3 Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Watambua nikienda au nikipumzika; wewe wazijua shughuli zangu zote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Watambua nikienda au nikipumzika; wewe wazijua shughuli zangu zote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Watambua nikienda au nikipumzika; wewe wazijua shughuli zangu zote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

3 Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, Umeelewa na njia zangu zote.

Tazama sura Nakili




Zaburi 139:3
21 Marejeleo ya Msalaba  

Hata maombolezo hayo yalipokwisha, Daudi akatuma mtu, akamtwaa, akamtia nyumbani mwake; naye akawa mkewe, akamzalia mtoto wa kiume. Lakini jambo lile alilolitenda Daudi likamchukiza BWANA.


Akaweka askari wenye kulinda ngome katika Edomu; katikati ya Edomu yote akaweka ngome, na Waedomi wote wakawa watumwa wa Daudi. Naye BWANA akampa Daudi ushindi kila kokote alikokwenda.


Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.


Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?


Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote ziko mbele zako.


Kama ningeyahesabu ni mengi kuliko mchanga; Niamkapo ningali pamoja nawe.


Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.


Ole wao wanaojitahidi kumficha BWANA mashauri yao, na matendo yao yamo gizani, nao husema, Ni nani atuonaye? Nani atujuaye?


Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri, nisimwone? Asema BWANA. Je! Mbingu na nchi hazikujawa nami? Asema BWANA.


Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.


Hata wakati wa chakula cha jioni; naye Ibilisi amekwisha kumtia Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti, moyo wa kumsaliti;


Naye alipokwisha kusema hayo, Yesu alifadhaika rohoni, akashuhudia akisema, Amin, amin, nawaambieni, Mmoja wenu atanisaliti.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo