Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Zaburi 101:5 - Swahili Revised Union Version

5 Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamwangamiza. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitamvumilia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

5 Anayemsengenya jirani nitamfutilia mbali; sitamvumilia mwenye majivuno na kiburi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

5 Anayemsengenya jirani nitamfutilia mbali; sitamvumilia mwenye majivuno na kiburi.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

5 Anayemsengenya jirani nitamfutilia mbali; sitamvumilia mwenye majivuno na kiburi.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

5 Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, huyo nitamnyamazisha; mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi huyo sitamvumilia.

Tazama sura Nakili

BIBLIA KISWAHILI

5 Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamwangamiza. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitamvumilia.

Tazama sura Nakili




Zaburi 101:5
25 Marejeleo ya Msalaba  

Ingawa BWANA yuko juu, anamjali mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.


Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala kumtenda mwenziwe mabaya, Wala kumsengenya jirani yake.


Maana Wewe wawaokoa watu wanaoonewa, Na macho ya kiburi utayadhili.


Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.


Usimshuhudie jirani yako uongo.


Usivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo.


Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.


Mwenye udaku hufunua siri; Basi, usishirikiane naye afunuaye midomo yake sana.


Mwenye kiburi na moyo wa majivuno, Taa yake ni dhambi.


Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu.


Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana.


Macho ya mwanadamu yaliyoinuka yatashushwa chini, na kiburi cha mwanadamu kitainamishwa, naye BWANA, yeye peke yake, atatukuzwa siku hiyo.


Wasingiziaji wamekuwamo ndani yako, ili kumwaga damu; na ndani yako wamekula juu ya milima; kati yako wamefanya uasherati.


Basi mimi, Nebukadneza, namhimidi Mfalme wa mbinguni, namtukuza na kumheshimu; maana matendo yake yote ni kweli, na njia zake ni za adili; na wale waendao kwa kutakabari, yeye aweza kuwadhili.


Usiende huku na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usijifaidi kwa damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.


Nawaambia, huyu alishuka kwenda nyumbani kwake amehesabiwa haki kuliko yule; kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.


Lakini, mambo yalivyo, niliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.


Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; wasiwe wachongezi; ila wawe watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.


Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wanaofundisha yaliyo mema;


Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa, Naye huyapima matendo kwa mizani.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo